• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI WA TABORA YAKAMILIKA NDANI YA MANISPAA YA SHINYANGA

Posted on: February 4th, 2022

Ziara ya siku mbili kwa Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Tabora imekamilika leo katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kutembea na kujifunza katika shughuli za uendeshaji wa miradi midogo na ya kati iliyopo katika eneo la Viwandani, uanzishwaji na utunzaji wa dampo lililopo Kizumbi uanzishwaji na uendeshwaji wa machinjio ya kisasa Ndembezi.

Akitoa salamu na ujumbe kutoka Manispaa ya Tabora, kaimu Mkurugenzi ndg Gudu Malulu aliwaeleza wenyeji kuwa lengo la kusafiri kwenda Shinyanga ni kujifunza namna ambavyo wamefanikiwa mambo mbalimbali kama yalivyotajwa hapo juu.

” Kwa dhati kabisa tumedhamiria kuja kujifunza na kuchukua yale yote yenye tija kubwa yatokanayo na ziara hii ili yaende kuwa msaada mkubwa kwa Manispaa yetu ya Tabora kwa muktadha wa kuipaisha Kiuchumi, kuboresha huduma za jamii, kuongeza na kuimarisha mapato na kimaendeleo kwa ujumla ili kufikia malengo ambayo Manispaa imejiwekea hasa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023”, alisema Malulu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg Jomaary Mrisho Satura alisema kuwa ni faraja sana kwa Wana Shinyanga kwa kutembelewa na ugeni kama huo muhimu jambo bora zaidi wenye lengo la kuja kujifunza mambo ambayo wameyaona ni mema kwao na yanapatika katika Manispaa ya Shinyanga, na kwamba aliwaahidi ushirikiano wa kutosha zaidi ili waridhike na wapate walichokusudia na kiende kuwa na matokeo chanya kwa wananchi wao.

Satura alisema kwamba Shinyanga siyo bora zaidi kuliko Halmashauri zingine, lakini kitendo cha Manispaa ya Tabora kuichagua Shinyanga ni jambo jema na lenye kuleta faraja kubwa sana, na kwamba Manispaa ya Shinyanga itakwenda kujifunza pia mambo mazuri kutoka Manispaa ya Tabora.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe Elias Masumbuko, aliwashukuru sana Waheshimiwa Madiwani Kutoka Manispaa ya Tabora kwa kuiona Shinyanga na hata wakaamua kwenda kujifunza, hivyo akawaomba kuwa huru kuuliza, kuhoji, kukosoa na kuboresha pale ambapo wanaona panafaa kwa kusudi la kuleta tija na kuwahudumia wananchi wa Manispaa ya Shinyanga.

“Siyo kwamba tuu mmekuja kujifunza kutoka kwetu, hapana nasi pia kupitia ujio wenu tutajifunza mambo mengi yaliyo mazuri zaidi ambayo mmekuja nayio na huenda sisi hatukuwa nayo pia, ndiyo maana nasema mkosoe, mshauri na mhoji kwa kadiri mtavyoona ili nasi tujikosoe pia,” alisema Meya Masumbuko.

Akifunga ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora, Mhe. Ramadhani Kapela aliwashukuru sana wana Shinyanga kwa ukarimu wao waliowapatia tangu kufika kwao hapo, ushirikiano waliowapatia kwenye ziara hiyo ya kujifunza mambo mbalimbali na kwamba akiwaahidi wajumbe wote kuwa watakwenda kuyafanyia kazi yote yale waliyojifunza ili yakalete mabadiliko chanya zaidi kwa wananchi wa Manispaa ya Tabora.

Kukamilika kwa ziara hiyo ya siku mbili katika Manispaa ya Shinyanga, kunatoa fursa sasa kwa wao Waheshimiwa Madiwani kwenda kuyachakata na kuyabadilisha yale yote waliyojifunza na kuyaona kwenye ziara hiyo ili yakaonekane kwenye madiliko ya vitendo na maisha ya wananchi wao wanaowaongoza kwenye maeneo yao, sambamba na kukuza pato la Manispaa, kuboresha huduma kwa jamii, kuibua na kusimamia miradi yao wenyewe.


Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndg Gudu Malulu (wa kwanza kushoto) akitoa salamu na ujumbe kutoka Manispaa ya Tabora wakati wa utambulisho kwenye ukumbi wa Mikutano Manispaa ya Shinyanga.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg Jomaary Satura (wa kwanza kushoto) akielezea jambo mbele ya wajumbe kabla ya kuanza ziara hawapo pichani.


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela akiwashukuru Waheshimiwa Madiwani wa Shinyanga, Menejimenti na wote walioshiriki kukamisha ziara hiyo.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga