• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MANISPAA YA SHINYANGA YAENDELEA KUWAWEZESHA WALIMU WA SEKONDARI KUTEKELEZA MTAALA MPYA WA ELIMU.

Posted on: January 22nd, 2026

Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, kwa kutambua umuhimu wa elimu katika maendeleo ya jamii, imeandaa mafunzo elekezi kwa walimu wa shule za sekondari kwa lengo la kuwajengea uelewa na kuongeza uwezo wao katika utekelezaji wa Mtaala Mpya Ulioboreshwa wa Elimu ya Sekondari.


Mafunzo hayo yamewakutanisha takribani walimu wawakilishi 170 kati ya walimu 496 kutoka shule 22 za sekondari zilizopo ndani ya Manispaa ya Shinyanga, hususan walimu wa masomo ya sayansi, sayansi ya jamii pamoja na elimu ya biashara.


Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo, Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Afisa Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi Mkoa wa Shinyanga, Ndg. Dedan Rutazika, ameipongeza Idara ya Elimu Sekondari ya Manispaa ya Shinyanga kwa kuendelea kuzingatia mabadiliko ya mitaala ya elimu na kuandaa mafunzo elekezi yanayolenga kuwajengea walimu uelewa na uwezo wa kutekeleza mitaala hiyo ipasavyo.


Kwa upande wake, Afisa Elimu Taaluma Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Richard Makoye, amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajengea walimu uelewa wa namna bora ya kuandaa na kutumia zana za kufundishia na kujifunzia, ili kuboresha ufundishaji wa masomo ya sayansi, sayansi ya jamii pamoja na elimu ya biashara kulingana na matakwa ya mtaala mpya.


Nao baadhi ya walimu walioshiriki mafunzo hayo wameishukuru Idara ya Elimu Sekondari kwa kuandaa mafunzo hayo, ambapo wamesema mafunzo hayo yamewasaidia kuongeza maarifa na uelewa wa mtaala ulioboreshwa, hususan katika masomo ya kidato cha kwanza na pili, hatua itakayochangia kuboresha ufaulu wa wanafunzi na kuwawezesha kufikia ndoto zao za kielimu.


Manispaa ya Shinyanga imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuinua ufaulu wa elimu ya sekondari, ikiongozwa na kaulimbiu yake isemayo “Shinyanga Municipal, Let Us Push Together.”

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MANISPAA YA SHINYANGA YAENDELEA KUWAWEZESHA WALIMU WA SEKONDARI KUTEKELEZA MTAALA MPYA WA ELIMU.

    January 22, 2026
  • KAMATI YA FEDHA NA UTAWALA MANISPAAYA SHINYANGA YAWATAKA WAKANDARASI KUIPA KIPAUMBELE MIRADI YA ELIMU.

    January 21, 2026
  • WANANCHI WAASWA KUEPUKA MIKOPO KAUSHA DAMU

    January 06, 2026
  • FUATILIA MATUKIO MBALIMBALI YA MANISPAA YA SHINYAGA KUPITIA MITANDAO YETU YA KIJAMII

    September 30, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga