• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

WANANCHI MANISPAA YA SHINYANGA WAASWA KUCHANGAMKIA MIKOPO YA ASILIMIA 7 ILI KUJIKWAMUA KIUCHUMI.

Posted on: May 14th, 2025

WANANCHI MANISPAA YA SHINYANGA WAASWA KUCHANGAMKIA MIKOPO YA ASILIMIA 7 ILI KUJIKWAMUA KIUCHUMI.


Na: Shinyanga MC


Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imetoa Elimu ya mkopo wenye riba nafuu, mikopo ya riba ya 7% yenye lengo la kuwawezesha wafanyabiashara wadogo wadogo, kujikwamua kiuchumi, kukuza mitaji yao na kuondokana na umaskini.


Akizungumza katika kikao cha wafanyabiashara kilichofanyika leo Mei 14, 2025 katika Soko la Ngokolo mtumbani, Mratibu na Msajili wa Wafanyabiashara Wadogo Mkoa wa Shinyanga, Bi. Rose Tungu, ameeleza kuwa mfanyabiashara yeyote mdogo anapaswa kuwa na kitambulisho cha ujasiriamali ili kunufaika na mkopo huu unaotolewa kuanzia kiasi cha shilingi 50,000 hadi shilingi milioni 4.


“Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameona si vyema wananchi kuendelea kutegemea mikopo ya ‘kausha damu’ ambayo huwasababishia usumbufu na msongo wa mawazo. Kwa kutambua hilo, amehakikisha mikopo ya asilimia 7 inapatikana kupitia Wizara yetu, ili kuwasaidia wafanyabiashara wadogo wadogo kuinuka kiuchumi bila changamoto kubwa ya marejesho,” amesema Bi. Rose.


Naye Bi. Vaileth Mambosasa kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi na wajasiriamali wadogo kujitokeza kwa wingi kuchangamkia mikopo hiyo ambayo inalenga kuwakwamua kiuchumi na kuwaondoa kwenye wimbi la umasikini.


Katika hatua nyingine, Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi kutoka Kitengo cha Makundi Maalum, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Ndg. David Malebeto, alisema kuwa kwa Manispaa ya Shinyanga pekee, kiasi cha shilingi milioni 140 kimetengwa kwa ajili ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo kupata mikopo hiyo.


Nao baadhi ya wajasiriamali wa Manispaa ya Shinyanga wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuthamini jitihada zao na kutoa mikopo hiyo ambayo imesaidia kuongeza mitaji yao, kuboresha maisha yao na kupambana na umasikini.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA YAPATA HATI SAFI UKAGUZI WA CAG 2023/2024

    June 12, 2025
  • MANISPAA YA SHINYANGA YATWAA VIKOMBE VITATU UMISSETA NGAZI YA MKOA 2025.

    June 10, 2025
  • MHE. MWEBEA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 05, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO OPD KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUKAMILIKA

    June 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga