• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

TAKUKURU MKOA WA SHINYANGA YATAMBULISHA RASMI PROGRAMU MPYA YA TAKUKURU RAFIKI

Posted on: February 14th, 2023

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga wametambulisha rasmi Programu ya TAKUKURU Rafiki ambayo inatajwa kuwa na mageuzi makubwa kwa wananchi na wadau ambao wataweza kishiriki katika kukabili tatizo la rushwa kwenye utoaji wa huduma kwa jamii na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Akiwaeleza wajumbe waliohudhuria utambulisho huo, Mkuu wa Dawati la Uelimishaji kwa Umma TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Bi. Helga Mfuruki alisema kuwa katika utekelezaji wa  programu hiyo ambayo inaakisi maana halisi ya nejo "rafiki" ambapo itabeba dhana ya kuwa na karibu kwa ushirikiano na wananchi pamoja na wadau mbalimbali kwa kutumia vikao ambavyo vitaitishwa nankuendeshwa katika ngazi ya Kata zote.

Helga alifafanua zaidi kuwa, mikutano ya hadhara itakuwa moja kati ya njia bora kabisa ya kuisogelea jamii na kuishirikisha katika kuzitambua na kuziibua kero ambazo zipo kwenye utoaji au upokeaji wa huduma kama vile Afya, Elimu ikiwa ni pamoja na namna mchakato wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta ya ujenzi wa miundombinu au maji.

"Aidha utambuzi wa kero hizo ni muhimu sana kwani zikiachwa pasipo kutatuliwa au kupatiwa ufumbuzi zinaweza kupelekea kutokea kwa vitendo vya rushwa jambo ambalo Takukuru isingependa kuendelea kutokea hasa katika utoaji wa huduma za ya elimu, afya, nk", alisisitiza Helga.

Kwa upande wake Mkuu wa Dawati la Uzuiaji Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Ndg. Reuben Chongolo alisema kuwa katika vikao hivyo ambavyo vitahudhuriwa na wananchi, viongozi wa kisiasa, watendaji wa serikali na wazabuni mbalimbali watashirikiana kwa pamoja katika kuzitatua kero hizo au kuweka mipango mikakati ya utatuzi wake kwa kushirikiana na TAKUKURU wenyewe.

Kufanikiwa vema kwa programu hiyo kutakuwa na faida zaidi katika kukuza ustawi wa Utawala Bora, kutaweza kuzuia vitendo vya rushwa visitokee kabisa kwenye utoaji wa huduma kwa umma na katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha faida nyinginezo ni pamoja na kuokoa fedha za umma ambazo zitaweza kutumika katika kujengwa kwa miradi bora zaidi, endelevu na yenye kukidhi thamani ya fedha iliyotumika.

"Mwisho kabisa TAKUKURU inapenda kutoa wito kwenu viongozi, watumishi na wananchi wote kwa ujumla kuwa sasa imekuja karibu zaidi nanyi katika sura ya rafiki zaidi  ili tushirikiane kuzuia vitendo vya rushwa visitokee katika utoaji wa huduma kwa umma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia programu hii ya TAKUKURU Rafiki", alisema Chongolo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MHE. MWEBEA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 05, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO OPD KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUKAMILIKA

    June 03, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO LA UTAWALA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUMALIZA UJENZI

    June 02, 2025
  • WANAFUNZI KUTOKA SHULE 20 ZA MANISPAA YA SHINYANGA WAKUTANA KUBADILISHANA UJUZI ILI KUBORESHA TAALUMA.

    May 17, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga