• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

Mzazi asiyetii wito wa kuitwa shuleni akamatwe

Posted on: May 12th, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mheshimiwa Josephine Matiro ameongoza mkutano wa wadau wa elimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna wa Manispaa. Wadau mbalimbali wa elimu katika Manispaa ya Shinyanga wamejadiliana mambo mbalimbali ya kuinua kiwango cha elimu kuanzia shule za awali, msingi, sekondari na chuo cha veta. Kwa pamoja waliazimia mambo mbalimbali ikiwemo kuwa kwa kila mzazi anapaswa kutii wito wa kuitwa shuleni kwa lengo la kutoa ushirikiano kwa walimu. Kwa jambo lolote ikiwemo masuala ya nidhamu za wanafunzi na mikutano mbalimbali ambayo uongozi wa shule utaona unafaa kuwaita wazazi, ni lazima wazazi waitikie wito huo bila kukosa. Mkutano uliazimia kuwa kwa mzazi asiyetii wito wowote kutoka katika shule ambayo watoto wao wanasoma, taarifa zitolewe mara moja katika vituo vya dola na mzazi huyo akamatwe.

Pamoja na agizo la kukamatwa kwa mzazi ayesitii wito wa shule, pia mkutano uliazimia kuanzia vituo vya elimu ya watu wazima ambayo itawasaidia wazazi na walezi kujifunza stadi za maisha kwa kushirikiana na chuo cha ufundi stadi cha VETA Shinyanga. Majadiliano yaliendelea pia katika eneo la upimaji wa walimu kwa kuwapa malengo ya ufaulu wa wanafunzi na kwa kila mkuu wa shule ambaye atashindwa kupanga na kusimamia utekelezaji wa malengo, atalazimika kuondolewa madaraka ya kuongoza katika shule hiyo.

Changamoto ya wanafunzi wa kike kupata ujauzito ni mada ambayo wadau wa elimu walichangia kwa muda mrefu na kuamua kuwa ipo haja ya mwanafunzi wa kike aliyepata ujauzito kuchukuliwa hatua za kisheria kama mtuhumiwa wa kuficha ushahidi iwapo atabainika kupotosha taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa mhusika alimpa mimba. Mkuu wa Wilaya alitoa ufafanuzi kuwa mahakama inapata wakati mgumu sana wa kutoa maamuzi kutokana na jamii ya wanashinyanga kuwa na tatizo la kutokukubali kutoa ushahidi mahakami pindi wanapotakiwa kufanya hivyo. "Haupo ushirikiano wa wazazi na binti mwenyewe aliyepewa ujauzito wakati wakitakiwa kutoa ushahidi mahakamani. Hali hii inachangia mashauri mengi kuchukua muda mrefu kutolewa hukumu ingawa suala hili lingeweza kupata ufumbuzi wa wahusika kupewa hukumu stahiki kama wazazi wa binti na binti mwenyewe wangetoa ushirikiano. Mahakama inafanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi. Upo mshikamano kwa wanajamii kulindana na kukataa kutoa ushahidi. Jamii ya namna hii inatakiwa kubadilika kwa ajili ya ukombozi wa watoto wetu wa kike". alieleza Mkuu wa Wilaya.

Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa Mwalimu Victor Emmanuel akijibu hoja zilizotolewa na wadau wa Elimu

Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa akijibu hoja mbalimbali za wadau wa elimu.

Naye Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa Mwalimu Victor Emmanuel alitoa ufafanuzi wa majukumu ya jamii kuwa ndio wamiliki wa shule zilizopo katika maeneo yao kwa kuwaambia kuwa suala la ulinzi wa mali za shule ni jukumu la wanajamii na si vinginevyo. Pamoja na ulinzi wa shule, pia jukumu la kuhakikisha wanafunzi wanapewa chakula cha mchana ni vema jamii kupitia kamati za shule kuomba kibali katika mamlaka, kibali ambacho kitawataka wazazi wachangie chakula cha watoto mashuleni."Shule ni ya jamii. Suala la ulinzi wa shule ni jukumu la jamii inayomiliki shule" Alisema Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa.

Afisa Elimu Msingi Mwalimu Yesse Kanyuma akiwasilisha mada mbele ya mkutano wa wadau wa elimu

Afisa Elimu Msingi wa Manispaa Mwalimu Yesse Kanyuma alisema kuwa serikali imewekeza fedha nyingi katika suala la ufundishaji wa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) ili kuhakikisha kuwa asiwepo mwanafunzi hata mmoja asiyejua kusoma, kuandika na kuhesabu afikapo darasa la tatu. Hii ina maana kuwa kwa kila mwanafunzi atakayehitimu elimu ya msingi asiwepo asiyekuwa na stadi za KKK. "Mkuu wa shule atakayeruhusu kuingia darasa la tatu mwanafunzi asiyejua kusoma, kuandika au kuhesabu, mwalimu mkuu huyo atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kushtakiwa mahakamani". Alisema Afisa Elimu Msingi wa Manispaa.

Sambamba na mkutano huo pia zawadi kwa washindi zilitolewa na Mkuu wa Wilaya alikuwa mgeni rasmi kuwatunuku washindi vyeti vya kufanya vizuri. Zawadi hizo zilitolewa kwa kuzingatia ufaulu wa shule na ufaulu wa wanafunzi. Kwa shule za sekondari, shule tatu bora za serikali na shule binafsi bora zilipewa vyeti vya ushindi kwa kufanya vizuri katika mitihani ya taifa iliyofanyika mwaka 2016. Shule za seikali ni shule ya sekondari Uhuru (3/22 kiwilaya, 12/103 kimkoa na 411/3280 kitaifa), masekelo 7/22 kiwilaya,25/103 kimkoa na 948/3280 kitaifa) na Chamaguha (8/22 kiwilaya,44/103 kimkoa na 1329/3280 kitaifa). Nazo shule binafsi zilizopata zawadi ya vyeti vya kufanya vizuri ni shule ya sekondari KOM (1/22 kiwilaya, 2/103 kimkoa na 83/3280 kitaifa), St. Francis of Asis (2/22 kiwilaya, 11/103 kimkoa na 353/3280 kitaifa) na Buluba (4/22 kiwilaya, 17/103 kimkoa na 513/3280 kitaifa). Pia wanafunzi watatu bora katika shule za sekondari za serikali na watatu bora katika shule za sekondari binafsi walizawadiwa vyeti vya kufanya vema.

Mwalimu Jasson Rwegasira akipokea zawadi ya cheti cha shule ya Uhuru kwa kuwa mshindi wa kwanza kiwilaya katika kundi la shule za sekondari za serikali.

Pia kwa upande wa shule za msingi, Jumla ya shule za msingi 15 zilipewa zawadi kwa mchanganuo wa shule 3 za serikali zilizofanya vizuri, shule 2 zisizo za serikali zilizofanya vizuri na shule 10 ambazo zimeonyesha maendeleo mazuri ya ufaulu wa wanafunzi katika mitihani iliyofanyika mwaka 2016 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2015. Kwa kutambua mchango wao wa kupanda juu katika viwango vya ufaulu wa wanafunzi, shule hizo 10 zilipewa vyeti ikiwa ni kuthamini juhudi walizozifanya ili waendelee kujitahidi zaidi kwa mwaka wa masomo wa 2017.

Mheshimiwa Mwendapole-Diwani wa kata ya Kambarage akichangia mada katika mkutano

Wadau mbalimbali wa Elimu wa Manispaa wakisikiliza mada zilizowasilishwa katika mkutano




Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MHE. MWEBEA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 05, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO OPD KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUKAMILIKA

    June 03, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO LA UTAWALA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUMALIZA UJENZI

    June 02, 2025
  • WANAFUNZI KUTOKA SHULE 20 ZA MANISPAA YA SHINYANGA WAKUTANA KUBADILISHANA UJUZI ILI KUBORESHA TAALUMA.

    May 17, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga