• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ATEMBELEA SOKO LA MBAO LA CHAMAGUHA PAMOJA NA SOKO LA MACHINGA KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WAFANYABIASHARA

Posted on: September 15th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga leo tarehe 15/09/2021 amefanya mkutano na wafanyabiashara wa soko la Chamaguha na soko la Machinga. Mkuu wa mkoa  aliongozana na Mkuu wa Wilaya, Mkurugerunzi wa Manispaa ya Shinyanga pamoja na Afisa Biashara, Afisa Maendeleo ya Jamii, Afisa Mipango Miji, Afisa Utumishi na Afisa TEHAMA.

 Mkutano ulifunguliwa na Mkuu wa Wilaya na baadaye kuwakaribisha wafanyabiashara kutoa changamoto zinazowakabili.

     Mwenyekiti Msaidizi wa soko la chamaguha alitoa  mojawapo ya changamoto ni miundombinu ya barabara kuwa mibovu na wakati wa masika kushindwa kutumika  hivyo kuomba kuboreshwa kwa wakati.hata hivyo Mwenyekiti huyo alimpongeza Mkurugenzi kwa kujitahidi kutatua changamoto nyingi zilizokuwa zikiwakabili.

Mkurugenzi wa Manispaa ya shinyanga alipata nafasi ya kuzungumza na wafanyabiashara na  kuwashukuru kwa kuhama kutoka soko la Kambarage bila shuruti, aliwaambia kuwa lengo kuu la Serikali ni kufanya biashara zao kukua na kuwa chachu ya maendeleo ya Manispaa ya Shinyanga.

Vivyo hivyo Mkurugenzi aliwaahidi kuwapa ushirikiano katika ukuaji wa soko kwa kuboresha miundombinu kama vile kuongeza idadi ya vyoo ili kuweza kutosheleza mahitaji ya wafanyabiashara pamoja na wateja kwa idadi.

Aidha katika mkutano huo Mkuu wa Mkoa alizungumza na wafanyabiashara na kuwashukuru kwa kukubali kuhama kutoka soko la Kambarage na kuhamia soko jipya la Chamaguha kwa kufuata ushauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan kwenye matumizi ya sera ya Diplomasia na Maelewano.

Mkuu wa Mkoa amemshukuru Mkuu wa wilaya, Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga na viongozi wengine kwa kuweka mazingira sawa mpaka soko kuanzishwa.

 Pia Mkuu wa Mkoa amesema kwa kushirikiana na Manispaa ya Shinyanga amewaahidi wafanyabiashara hao kuendelea kuwaboreshea miundombinu ya soko hasa kwa kuanza na urekebishaji wa  barabara ili kuwe na mazingira mazuri ya kufanyia biashara zao.

Pia Mkuu wa Mkoa aliwahakikishia wafanyabiashara wote katika soko la mbao la Chamaguha kuwa eneo hilo ndilo litakalokuwa eneo pekee la kuuza mbao pamoja na bidhaa za mazao ya misitu.

Akiwa katika soko la Machinga lililopo kata ya mjini, Mkuu wa Mkoa alikutana na wafanyabiashara ambao pia alisikiliza kero zao ikiwa ni Pamoja na ukosefu wa maji, miundombinu mibovu ya barabara, vibanda vya wafanyabiashara kutokuwa na ubora na kuhofia changamoto kubwa wakati wa masika, pia waliomba kuwepo na mnada siku ya jumatano ya kila wiki.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa aliwapa moyo wafanyabiashara hao kwa kuahidi kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kutatua changamoto zao zote. Aliwaahidi kulitangaza soko hilo kuwa rasmi na kulifanyia ufunguzi.

Viongozi wa soko la Machinga waliwasisitiza wafanyabiashara wenzao kutimiza majukumu yao kwa kulipia vitambulisho vya wajasiriamali wadogo ili kufanya kazi katika mazingira yasiyokuwa na bugudha ama usumbufu.

MATUKIO KATIKA PICHA


Soko la mbao Chamaguha

Mkuu wa Mkoa akisikiliza Wafanyabiashara

Wafanyabiashara wakisikiliza kwa makini

Mkuu wa Mkoa akitembelea soko la mbao

Soko la Machinga

Mkuu wa Mkoa akisikiliza changamoto za

Wafanyabiashara wa soko la Machinga

Mkuu wa mkoa akitembelea Soko la Machinga

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga