• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MKURUGENZI MANISPAA YA SHINYANGA AWAAGIZA VIONGOZI WA ELIMU KUHAMASISHA JAMII

Posted on: August 26th, 2023

Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule na Walimu wakuu katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wametakiwa kuhakikisha wanafunzi wote wa Shule za Msingi na Sekondari katika Halmashauri hiyo wanapata chakula Shuleni kwa kuhamasisha wazazi na walezi kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao  ili kuwapa utulivu wa kujifunza wawapo shuleni.

Maelekezo hayo yametolewa jana, Agosti 25, 2023 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Mwalimu Alexius Revocatus Kagunze wakati anaongea na Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule za Sekondari wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwenye Mkutano wa kawaida wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) Manispaa ya Shinyanga uliofanyika katika Shule ya Sekondari Buluba mjini Shinyanga.

"Upatikanaji wa Chakula Shuleni ni moja ya utekelezaji wa KPI (vigezo vya upimaji) za mikataba yenu mliyojaza kwa ajili ya kusimamia taaluma shuleni. Chakula shuleni ni muhimu sana kwa ajili ya kuleta utulivu kwa mwanafunzi kujifunza anapokuwa darasani. Nawaagiza kuhakikisha mnaitisha vikao vya wazazi kuhamasisha wazazi kuwachangia watoto wao chakula shuleni." Alisisitiza Kagunze.

Kuhusu usafi na utunzaji wa mazingira, Kagunze amewaelekeza Wakuu wa Shule na Walimu wakuu kuhakikisha mazingira ya Shule zao yanakuwa safi muda wote na kukitumia kipindi hiki cha kiangazi  kuandaa mashimo ambayo watapanda miti ya kutosha pindi msimu wa mvua utakapoanza.

"Tumieni kipindi hiki cha kiangazi kuandaa mashimo kwa ajili ya kupanda miti mingi msimu wa mvua utakapoanza. Yaandaeni vizuri, mtie mbolea na inasisitizwa kuwa tupande miti ya matunda ya kutosha pamoja na ya kimvuli pia. Aidha, tuendelee kuitunza miti ambayo tumekwisha ipanda ili kutunza mazingira yetu." Aliongeza Kagunze.

Wakati huo huo, Mkurugenzi Kagunze amewataka viongozi wa elimu hususani Walimu wakuu na Wakuu wa Shule kujenga umoja, upendo na ushirikiano huku wakitenda haki kwa walimu wote wanaowaongoza katika Shule zao.

Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) ulianzishwa mwaka 2005 ukiwa na malengo ya kuwakutanisha Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa uongozi mashuleni. Kwa mujibu wa Katiba ya Umoja huo, muundo wake umegawanyika katika ngazi ya Halmashauri, Mkoa, Kanda na Taifa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga