• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MKATABA WA MILIONI 300 WASAINIWA KATI YA MANISPAA NA VETA KWA AJILI YA UTENGENEZAJI WA MADAWATI 2500 KWA SHULE ZA MSINGI NA VITI NA MEZA 2500 KWA SHULE ZA SEKONDARI

Posted on: October 31st, 2021

Madawati 2500 kwa shule za msingi, viti na meza 2500 kwa shule za sekondari itawezesha wanafunzi wote kuanzia chekechea hadi Sekondari kukaa katika madawati.hii inakwenda sambamba na kumsapoti Rais wetu mama Samia ambae amekuwa na msukumo mkubwa katika utoaji huduma kwa jamii, ambapo sh trillion 1.3 zilizotolewa katika mpango wa covid19  Manispaa imepokea million 880 kwa ajili ya ukamilishaji wa madarasa 35 kwa shule za sekondari na madarasa 9 kwa shule shikizi.Katika kumuunga mkono mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Manispaa ya Shinyanga imetumia mapato yake ya ndani kutengeneza madawati 2500 kwa shule za msingi, viti na meza 2500 kwa shule za sekondari.ambapo Mwenyekiti wa Wafanyabiashara ndg Shuma alialikwa ili ashuhudie kuwa sehemu ya fedha wanayotoa wafanyabiashara kama kodi inatumika kwa ajili ya maendeleo. Utengenezaji wa madawati , viti Pamoja na meza utatoa fursa kwa wanafunzi Zaidi ya 50 wa VETA katika fani ya useremala na uchomeleaji  kujifunza kwa vitendo.

Mchakato wa kutengeneza madawati uliwashirikisha wanajamii wote na ulipitia michakato yote ya manunuzi na VETA wakaibuka kidedea kwa kuwa wao ndo walikuwa the lowest bider na pia wana miundo mbinu ya kisasa ya Serikali katika kufanya kazi hiyo.

Mkuu wa Chuo cha VETA ametoa shukrani zake kwa uongozi wa Manispaa kwa kukubali kufanya kazi Pamoja.

Mwenyekiti wa Kamati za Huduma, Uchumi, Elimu na Afya Mheshimiwa Nkwabi alifurahishwa na mkataba huo wa ujenzi wa madawati ambapo alisema ile ndoto ya kuwa wa kwanza kitaifa inaenda kutimia na ndoto ya Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kuwa jiji pia inaenda kufanikiwa.” Mkuu wetu, zile ndoto za Halmashauri ya Shinyanga kuwa jiji zinaenda kutimia, tunapotoa ujinga sasa ni dalili njema kuwa tunaelekea kwenye mafanikio”. Alisema Mheshimiwa Nkwabi.Alimaliza kwa kutoa shukrani zake na kuahidi kuwa kamati itatoa ushirikiano mkubwa kwa Mkurugenzi Pamoja na ofisi ya Mkuu wa Wilaya kuhakikisha mikakati yote ya maendeleo inafanikiwa kwa ufanisi mkubwa.

Pia Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Ndg. Shuma Madulu alitoa shukrani zake kwa Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya kwa kuonyesha uwazi katika masuala yote yahusuyo maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga. “Nimshukuru Mkurugenzi, kwa sababu Wakurugenzi waliopita Shinyanga ni wengi lakini kwa utandawazi huu amekuja kutuonyesha wafanyabiashara kushuhudia na kutukumbuka kuwa nasi ni wachangiaji wakuu katika maendeleo kitu ambacho hapo nyuma hakikuwahi kufanyika. Naomba Mkurugenzi aendelee Pamoja na Mkuu wetu wa Wilaya ambae amekuwa akisisitiza maendeleo akiamini Maendeleo ndani ya Shinyanga yetu yanawezekana”. Alisema Ndg Shuma.

Aidha kwa nyakati tofauti, Afisa Elimu Msingi na Sekondari Walitoa shukrani zao za dhati hasa wakizingatia kuwa miradi hiyo inawalenga wao moja kwa moja.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mheshimiwa Makune alitoa shukrani zake kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia kwa kuleta fedha kwa ajili ya mipango ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, kisha akapata wasaa wa kumkaribisha Mkuu wa Wilaya Bi Jasinta Mboneko ili aseme machache kabla ya tukio la kusaini mkataba kuanza.

Mkuu wa Wilaya alianza kwa kuipongeza Halmashauri kwa hatua nzuri na Madhubuti ya kuhakikisha Miundo mbinu ya darasani inaimarika na kwamba kila mwanafunzi anakaa kwenye dawati ili kufanya zoezi la kujifunza liwe Rafiki kwa wanafunzi na walimu pia alimpongeza Mkurugenzi Pamoja na Kamati za Huduma, Uchumi, Elimu na Afya kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuleta Maendeleo. “Tukiacha wanafunzi twende kwa Walimu kwa sababu na wao katika mazingira ya Ufundishaji lazima wakae sehemu nzuri, kwa kuzingatia hilo mimi binafsi kama mkuu wa Wilaya nimekwishaanza kupeleka Meza na viti katika baadhi ya shule”. Alisema Bi. Mboneko. Alisisitiza Walimu kutoa majaribio kila wiki ili kuwaandaa Watoto wasiogope mitihani na kuwafanya wapate ufaulu mzuri.  

Baada ya Hotuba fupi ya Mkuu wa Wilaya Mkataba ulisainiwa na pande zote.

Hafla hiyo fupi ya utiaji Saini mkataba huo ilifanyika katika ukumbi wa VETA tarehe 28 Oktoba 2021 Alhamisi huku ikishuhudiwa na Wataalamu kutoka Manispaa, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara, Mkuu wa Wilaya, Mstahiki Naibu Meya, Mwenyekiti wa Kamati za Huduma, Uchumi, Elimu na Afya na baadhi ya Watumishi kutoka VETA.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga