- Mwanzo
- Kuhusu sisi
- Utawala
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma Zetu
- Madiwani
- Miradi
- Machapisho
- Kituo cha Habari
Jumla ya Miradi nane (08) yenye thamani ya Tsh. 1,344,653,360 imepitiwa na Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga tarehe 11.05.2019. Miradi hii inajumuisha ya Halmashauri (Tsh.39,020,260), Serikali kuu (Tsh.310,472,100), Sekta Binafsi (Tsh.750,000,000) na mchango wa wadau (Tsh.245,161,000). Ukiwa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Mwenge wa Uhuru umekimbizwa umbali wa kilometa 102.5, katika Kata ya Kizumbi (Miradi miwili), kata ya Masekelo (Mradi mmoja), kata ya Mwawaza (Mradi mmoja), kata ya Ibadakuli (Miradi miwili) na kata ya Mjini (Miradi miwili), kuzindua na kuona miradi mbali mbali.
Aidha miradi hiyo iliyozinduliwa na kuonwa na Mwenge ni:
Miradi yote iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru ilikubalika kwa asilimia 100 na kufunguliwa.
Mwenge wa Uhuru umekabidhiwa leo tarehe 12.05.2019 katika wilaya ya Kishapu.
Tazama picha za matukio ya Mwenge hapa chini

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga akiwa na kamati yake ya Mwenge wakiusubiri Mwenge wa Uhuru kutoka Halmashauri ya Msalala

Mkuu wa Wilaya ya Kahama akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa wilaya ya Shinyanga katika Manispaa ya Shinyanga

Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga akiwa amebeba Mwenge wa Uhuru

Mchungaji akiwakabidhi wakimbiza Mwenge pamoja na watu wote mikononi mwa Mungu kwa sala fupi ili zoezi lifanyike kwa amani

Sheikh wa wilaya akiomba dua njema katika kuukaribisha Mwenge wa Uhuru

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akikagua mradi wa ufugaji wa samaki katika moja ya mabwawa katika mradi huo

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akipanda mti aina ya Royal Palm katika kuunga juhudi za uhifadhi wa mazingira

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ufugaji wa samaki na uhifadhi wa mazingira ktk kata
ya Kizumbi kijiji cha Nhelegani

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akiwasikiliza kwa makini kikundi cha vijana kinachokemea rushwa ya ngono VETA Shinyanga

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akisikiliza ripoti kutoka kwa Mkurugenzi wa Kituo cha Mafuta GILITU PETROLEUM STATION

Jiwe la msingi lililosimikwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa ktk Kituo cha Mafuta GILITU PETROLEUM STATION

Mmoja wa watumbuizaji katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Manispaa ya Shinyanga


Afisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Shinyanga akitoa ripoti ya Mradi wa Vyumba vitano vya madarasa katika s/m Viwandani

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akiweka jiwe la msingi katika S/m Viwandani baada ya kuridhishwa na mradi


Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akikagua mradi wa Tarafa ya Ibadakuli

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akitoa sifa kemkem katika mradi wa Jengo la Tarafa ya Ibadakuli

Mradi wa maji

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akiweka jiwe la msingi katika mradi wa maji



Mganga Mkuu wa Manispaa akitoa ripoti ya Mradi wa uboreshaji Zahanati ya Mwawaza kwa kujenga jengo jipya la maabara


Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akikagua jengo la maabara katika Zahanati ya Mwawaza

Kamishna wa Polisi akitoa ripoti ya Mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari Polisi



Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akifungua kwa kuweka jiwe la msingi Mradi wa Nyumba za Askari Polisi


Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akiwa na wanafunzi wa shule ya Sekondari Uhuru

Mradi wa pikipiki

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akionyeshwa document za pikipiki katika mradi wa kikundi cha vijana wamiliki na waendeshaji
wa pikipiki maarufu kama bodaboda

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akikagua mabanda yaliyokuwa na shughuli mbalimbali ktk uwanja wa Sabasaba




Mkuu wa wilaya ya Shinyanga (kushoto) akikaribishwa na mwenyeji wake Mkuu wa wilaya ya Kishapu alipokwenda kukabidhi Mwenge
wa Uhuru baada ya zoezi la kukagua miradi katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kumalizika.

Tanesco S, Mwanza Road
Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga
Simu: +255-28-2763213
Simu ya Mkononi: 0759 023 788
Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz
Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga