• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

Miradi ya Shilingi Bilioni 1.3 yapitiwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 Manispaa ya Shinyanga

Posted on: May 12th, 2019

Jumla ya Miradi nane (08) yenye thamani ya Tsh. 1,344,653,360 imepitiwa na Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga tarehe 11.05.2019. Miradi hii inajumuisha ya Halmashauri (Tsh.39,020,260), Serikali kuu (Tsh.310,472,100), Sekta Binafsi (Tsh.750,000,000) na mchango wa wadau (Tsh.245,161,000). Ukiwa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Mwenge wa Uhuru umekimbizwa umbali wa kilometa 102.5, katika Kata ya Kizumbi (Miradi miwili), kata ya Masekelo (Mradi mmoja), kata ya Mwawaza (Mradi mmoja), kata ya Ibadakuli (Miradi miwili) na kata ya Mjini (Miradi miwili), kuzindua na kuona miradi mbali mbali.

Aidha miradi hiyo iliyozinduliwa na kuonwa na Mwenge ni:

  • Mradi wa Ufugaji wa Samaki na Hifadhi ya Mazingira (MWANANCHI FARM)
  • Mradi wa kituo cha Mafuta (GILITU PETROLEUM STATION)
  • Mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na Kitongoji cha Ishoshandili
  • Mradi uboreshaji zahanati ya Mwawaza kwa kujenga jengo jipya la Maabara
  • Mradi wa ujenzi wa vyumba vitano (05) vya madarasa katika Shule ya Msingi Viwandani
  • Mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari Polisi
  • Mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Tarafa ya Ibadakuli
  • Mradi wa kikundi cha vijana wamiliki na waendeshaji wa Pikipiki

Miradi yote iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru ilikubalika kwa asilimia 100 na kufunguliwa.

Mwenge wa Uhuru umekabidhiwa leo tarehe 12.05.2019 katika wilaya ya Kishapu.


Tazama picha za matukio ya Mwenge hapa chini

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga akiwa na kamati yake ya Mwenge wakiusubiri Mwenge wa Uhuru kutoka Halmashauri ya Msalala

Mkuu wa Wilaya ya Kahama akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa wilaya ya Shinyanga katika Manispaa ya Shinyanga

Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga akiwa amebeba Mwenge wa Uhuru

Mchungaji akiwakabidhi wakimbiza Mwenge pamoja na watu wote mikononi mwa Mungu kwa sala fupi ili zoezi lifanyike kwa amani

Sheikh wa wilaya akiomba dua njema katika kuukaribisha Mwenge wa Uhuru

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akikagua mradi wa ufugaji wa samaki katika moja ya mabwawa katika mradi huo

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akipanda mti aina ya Royal Palm katika kuunga juhudi za uhifadhi wa mazingira

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ufugaji wa samaki na uhifadhi wa mazingira ktk kata

ya Kizumbi kijiji cha Nhelegani

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akiwasikiliza kwa makini kikundi cha vijana kinachokemea rushwa ya ngono VETA Shinyanga

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akisikiliza ripoti kutoka kwa Mkurugenzi wa Kituo cha Mafuta GILITU PETROLEUM STATION

Jiwe la msingi lililosimikwa na Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa ktk Kituo cha Mafuta GILITU PETROLEUM STATION

Mmoja wa watumbuizaji katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Manispaa ya Shinyanga

Afisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Shinyanga akitoa ripoti ya Mradi wa Vyumba vitano vya madarasa katika s/m Viwandani

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akiweka jiwe la msingi katika S/m Viwandani baada ya kuridhishwa na mradi

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akikagua mradi wa Tarafa ya Ibadakuli

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akitoa sifa kemkem katika mradi wa Jengo la Tarafa ya Ibadakuli 

Mradi wa maji

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akiweka jiwe la msingi katika mradi wa maji

Mganga Mkuu wa Manispaa akitoa ripoti ya Mradi wa uboreshaji Zahanati ya Mwawaza kwa kujenga jengo jipya la maabara

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akikagua jengo la maabara katika Zahanati ya Mwawaza

Kamishna wa Polisi akitoa ripoti ya Mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari Polisi

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akifungua kwa kuweka jiwe la msingi Mradi wa Nyumba za Askari Polisi 

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akiwa na wanafunzi wa shule ya Sekondari Uhuru

Mradi wa pikipiki

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akionyeshwa document za pikipiki katika mradi wa kikundi cha vijana wamiliki na waendeshaji

wa pikipiki maarufu kama bodaboda

Kiongozi wa mbio za  Mwenge kitaifa akikagua mabanda yaliyokuwa na shughuli mbalimbali ktk uwanja wa Sabasaba 

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga (kushoto) akikaribishwa na mwenyeji wake Mkuu wa wilaya ya Kishapu alipokwenda kukabidhi Mwenge 

wa Uhuru baada ya zoezi la kukagua miradi katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kumalizika.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga