• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MIAKA MIWILI YA MH DKT. SAMIA SHINYANGA YAKUSANYA BIL 255 ZA MADINI

Posted on: March 25th, 2023

MKOA wa Shinyanga umekusanya zaidi ya shilingi Bilioni 255 kama mapato yatokanayo na shughuli za Madini, katika kipindi cha miaka miwili ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan madarakani.

Hayo yamebainishwa leo Machi 25, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mh. Christina Mndeme katika Kongamano la miaka miwili ya mafanikio ya Utawala wa Rais Samia lililofanyika leo Machi 25, 2023 katika ukumbi wa Mikutano wa Jengo la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali, wakiwamo na Wabunge wa Mkoa wa Shinyanga.

Mh. Mndeme ameeleza kuwa Makusanyo hayo yanahusisha ada za leseni, mrabaha na ada za ukaguzi zinazokusanywa kupitia Wizara ya Madini.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Shinyanga umetoa leseni mbalimbali za madini 827 katika kipindi hicho cha miaka miwili.

Ameongeza kuwa vituo viwili vya ununuzi wa madini vimeanzishwa ikiwa ni mkakati wa kusogeza huduma za biashara ya madini karibu na maeneo ya wachimbaji wadogo.

Mndeme ametoa taarifa hiyo wakati wa kongamano la kuangazia mafanikio yaliyopatikana mkoani Shinyanga ndani ya kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika hatua nyingine, Mh. Mndeme amesema Mkoa wa Shinyanga umefanikiwa kujenga vyumba vipya vya madarasa 833, mabweni 3 na matundu ya vyoo 1,003 katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akielezea mafanikio ya miaka miwili ya Rais Samia.

Amesema “Mkoa umepokea zaidi ya shilingi Bilioni 37.68 katika sekta ya elimu na kufanikiwa pia kukarabati shule kongwe mbili za msingi”.

Amesema zaidi ya shilingi Bilioni 3.18 zimetumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa 108, mabweni 3, matundu ya vyoo 1,002 na kukarabati shule kongwe mbili za msingi.

Amesema “shilingi Biliioni 20.32 zimetuika kujenga shule mpya 7, vyumba vya madarasa 725 kwa shule za sekondari, shilingi bilioni 11.96 zimetumika kugharamia elimu bila ada na shilingi bilioni 2.21 zimetumika katika ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Wilayani Kishapu”.

Aidha, katika Utawala wa miaka miwili ya Rais, Dkt. Samia, Mh. Mndeme amesema Mkoa wa Shinyanga umejenga viwanda vipya 108 katika kipindi cha miaka miwili kuanzia mwezi Machi mwaka 2021 hadi mwezi Februari mwaka huu  na kuufanya kufikisha jumla ya viwanda 838.

Kabla ya kujengwa kwa viwanda hivyo vipya, mkoa huo ulikuwa na viwanda 730, lakini kutokana na fursa za uwekezaji zilizofunguliwa na Serikali ya awamu ya sita viwanda 108 zaidi vimejengwa katika mkoa huo ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.79.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi akielezea mafanikio ya miaka miwili ya Rais Samia katika Wilaya ya Shinyanga.

Viwanda vingi ni vile vinavyoongeza thamani ya mazao ya kilimo na mifugo pamoja na uchimbaji wa madini ya dhahabu na almasi.

Mbali na Mh. Mdeme, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mh. Johari Samizi, amebainisha kuwa katika Utawala wa Miaka miwili ya Mama Samia, ndani ya Wilaya ya Shinyanga, Miradi ya Ujenzi wa Masoko ikiwemo Soko la Ibinzamata, Ngokolo Mtumbani na Soko Kuu inayotekelezwa na Mapato ya Ndani kutoka Halmashauri ya manispaa ya Shinyanga inaendelea, halikadhalika Ujenzi wa Vituo vya Afya ikiwamo Ihapa na Kambarage ambayo Serikali imewezesha kujenga ili kuongeza ufanisi wa huduma.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MHE. MWEBEA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 05, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO OPD KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUKAMILIKA

    June 03, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO LA UTAWALA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUMALIZA UJENZI

    June 02, 2025
  • WANAFUNZI KUTOKA SHULE 20 ZA MANISPAA YA SHINYANGA WAKUTANA KUBADILISHANA UJUZI ILI KUBORESHA TAALUMA.

    May 17, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga