• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MANISPAA YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: May 4th, 2023

Na. Shinyanga MC

Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imepongezwa kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo mpaka kufikia Aprili, 2023 Manispaa imekusanya zaidi ya Bilioni 5 sawa na asilimia 108 dhidi ya lengo la asilimia 100 iliyokadiriwa.

Pongezi hizo zimetolewa leo terhe 4 Mei, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi alipokuwa akitoa salamu za Serikali katika Mkutano wa Baraza la Madiwani lililofanyika katika Ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliopo Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanya.

"Nichukue fulsa hii kuwapongeza sana Uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ukiongozwa na Mstahiki Meya Mhe. Elias Masumbuko kwa upande wa Madiwani na Ndg. Jomaary Satura kwa upande wa Menejimenti na watumishi wote wa Manispaa kwa namna ambavyo mnafanya kazi kwa umoja, juhudi, maarifa na ubunifu mkubwa katika kukusanya mapato ya Serikali hadi kufikia Aprili 2023 tayari mmevuka  lengo la mwaka, hongereni sana kwa hatua hii", alisema Mhe. Johari.

Pamoja na pongezi hizo lakini Mhe. Johari alisisitiza zaidi katika ubunifu, bidii na nidhamu ya fedha za Serikali na katika uongezaji wa vyanzo vya mapato ili kuongeza wigo wa ukusanyaji na utekelezaji wa miradi ya maendeleo iweze kutekeleze kwa kasi zaidi jambo ambalo litawaletea maendeleo wananchi ambao ndiyo wenye miradi na fedha zao.

Aidha alikumbusha juu ya umuhimu wa kutunza mazingira, vyanzo vya maji na usafi kwa ujumla kwakuwa Tanzania kama Nchi inajumuika na nyingine katika kupambana na masuala ya Tabia Nchi jambo ambalo ni Ajenda ya dunia kwa sasa. Huku akiwaeleza kuwa kuna ujio wa Mwenge wa Uhuru ambao unayo Kauli Mbiu inayosisitiza utunzaji wa mazingira na kwa Manispaa Mwenge utapokelewa tarehe 28 Julai, 2023.

Awali Ndg.Mensaria Mrema (Afisa Mipango) akisoma taarifa ya utekelezaji kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa alisema kwa kipindi cha robo ya 3, 2023 Manispaa imepokea Tzs. 1, 715, 900,000/ ikiwa ni fedha za bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Elimu na ujenzi wa nyumba za viongozi.



Picha ikimuonesha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga (aliyesiama) akitoa ufafanuzi wa jamho wakati mkutano wa Baraza la Madiwani  Mei 4, 2023 katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliyopo Ofisi ya  Mkurugenzi wa Manispaa.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg. Jomaary Mrisho Satura akimkaribisha Mstahiki Meya kwa ajili Itifaki ya Mkuu wa Wilaya mapema leo katika mkutano wa Madiwani.

Muonekano wa baadhi ya waheshimiwa madiwani kaika picha ya ukumbini kahla ya kuanza kwa mkutano.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga