• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MANISPAA YA SHINYANGA YAENDESHA MAFUNZO YA MFUMO WA MSHITIRI KWA WAGANGA WAFAWIDHI WA HOSPITALI, VITUO VYA AFYA, ZAHANATI NA WATUNZA STOO ZA DAWA.

Posted on: April 15th, 2023

Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imeendesha mafunzo wa ya mfumo wa MSHITIRI (mjaziaji bidhaa za afya zilizopungua kutoka Bohari ya Dawa Taifa - MSD) kwa Waganga Wafawidhi wa Hospitali, Vituo vya Afya, Zahanati na watunza Stoo za Dawa wote kwa lengo la kuwezesha ili waweze kusimamia, usambazaji na udhibiti mzuri wa dawa katika maeneo yao ya kiutendaji.


Akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg. Jomaary Mrisho Satura aliwaeleza wataalamu hao kuwa Serikali inayo dhamira njema sana kwa wataalamu na wananchi wote kwa ujumla ndiyo maana ikaamua kuja na mfumo huu ambao ukitekelezwa kwa umakini na uzalendo mkubwa itaweza kuisadia Serikali kuondoa urasimu, ufujaji na hivyo wananchi watanufainka na mfumo huu kama lengo la Serikali lilivyo.


"Serikali imeamua kuboresha eneo hili la utoaji wa dawa kwenu wataalamu na mawakala ili kuweza kutoa huduma kwa urahisi na kwa wakati, kuondoa uwezekano wa msimamizi au wakala kuingia matatizoni, kuondoa urasimu ambao awali ulikuwepo kwakuwa hivi sasa ataomba kupitia mfumo, na mwisho kabisa lengo kusidiwa la Serikali litakuwa limefikiwa kikamilifu," alisema Satura.


Awali akimkaribisha kufungua mafunzo hayo, Mtunza Stoo za Dawa Ndg. Charles Malogi alisema kwamba Manispaa ya Shinyanga inatekeleza maelekezo ya Serikali ambapo baadhi ya wataalamu walialikwa kuhudhuria mafunzo ya mfumo huo yaliyofanyika ngazi ya Mkoa ambapo walielekezwa na wao kushusha chini mafunzo hayo kwa wataalamu ambao ni Waganga Wafawidhi wa Hospitqli, Vituo vya Afya, Zahanati na watunza Stoo za Dawa wote wa Manispaa tukio ambalo ndiyo linafanyika leo tarehe 15 Machi, 2023.


Malogi aliwataka wataalamu kuupokea mfumo huu kwa mikono miwili kwakuwa unakuja na suluhisho la kudumu dhidi ya malalamiko yaliyokuwa yakitolewa awali, huku akiwataka kwenda kuutekeleza kwa uzalendo na ufanisi ili uweze kuleta matokeo chanya kwa walengwa amabo ndiyo wananchi na ndiyo walipa kodi wa Nchi hii.


"Twendeni tukautekeleze mfumo huu kwa vitendo huku tukitanguliza uzalendo na ufanisi katika kuwahudumia wananchi wetu, na ndiyo maana tupo hapa na kwamba tumemualika Mkurugenzi wa Manispaa ili aje atoe nasaha zake kenu kwakuwa naye ni sehemu ya Serikali ambaye anayo dhamana kubwa kwa Majispaa ya Shinyanga, tuupokee mfumo huu kwa mikono miwili tukautekeleze ipasavyo," alisema Malogi


Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga inakeleza Mfumo huu wa MSHITIRI ambao unakwenda kuwasaidia wataalamu kusimamia AFUA mbalimbali za mfumo wa Ugavi wa Bidhaa za Afya ikiwamo kufanya Medicine Audit mara kwa mara katika vituo vya kutolea huduma kwa ajili ya kupunguza changamoto zitokanazo na usimamizi mbovu wa bidhaa za afya.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga