• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MANISPAA YA SHINYANGA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUGAWA MITUNGI YA GESI 39

Posted on: March 10th, 2023

HALMASHAURI ya Manispaa ya Shinyanga ni miongoni mwa Halmashauri Nchini iliyoshiriki kikamilifu katika kuadhimisha kilele cha Sherehe za Siku ya Wanawake Duniani ambayo Kimkoa ilifanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Machi 8, 2023.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi 39.

Akizungumza wakati wa Sherehe hizo, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, aliseama kuwa wanawake ni kundi kubwa lenye nguvu zaidi katika nyanja mbalimbali ikiwamo Uongozi, Uchumi, Kijamii na kadhalika hivyo katika kuadhimisha siku yao ni muhimu sana wakapongezwa na kupewa nguvu zaidi ili wakaongeze jitihada.

Hivyo basi katika kuhakikisha kuwa Serikali inawajali na kuwaongezea nguvu kwa kuwapatia mitungi ya Gesi bure kabisa jambo ambalo litaenda kuboresha na kuongeza tija kwa shughuli zao za kila siku katika kujipatia kipato cha familia zao na Taifa pia, kwani wataondokana na matumizi ya mkaa au kuni jambo ambalo linatumia muda mrefu zaidi katika kupika kulinganisha na matumizi ya Gesi.

“Ukitazama hasa katika kipindi hiki Wanawake wamekuwa na mchango mkubwa sana katika jamii zetu na Nchi kwa ujumla kama ambavyo unamuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi bora zaidi, kuna Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Tulia Akson anaongoza vema kabisa Bunge letu na wengine wengi zaidi Tanzania na nje ya Nchi hii ni kielelezo kuwa wanawake ni kundi kubwa na muhimu zaidi.

"Kwa msingi huu sasa nawapongeza sana Manispaa ya Shinyanga kwa kuamua kuwapatia mitungi ya gesi bure kwa wanawake wajasiriamali wao kutoka katika Kata zao zote 17 za Manispaa, jambo ambalo ni la kuigwa na Halmashauri nyingine kwani watakuwa wanakwenda na Kauli Mbiu isemayo Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia, Chachu katika kuleta Usawa wa Kijinsia maana yake Manispaa wamekuwa wabunifu na kuwaletea mabadilko wajasiriamali wao ambayo ni chachu kwao " alisema Mhe. Mkude.

Mhe. Mkude aliwakumbusha pia wananchi wote waliofika katika sherehe hiyo juu ya umuhimu wa kuchukua tahadhari zaidi kwa ugonjwa wa Homa Kali na Joto yaani UVIKO 19 kwani ugonjwa huo upo na kwamba kwa wale ambao hawajamalizia Chanjo ya pili wafanye hivyo haraka kutoka na umuhimu wake.

"Tuendelee kuchukua tahadhari zaidi kwa ugonjwa huu, na ikumbukwe kwamba hakuna madhara yoyote kwenye Chanjo hizo zinazotolewa na Serikali kupitia Sekta ya Afya katika vituo vyote vya Afya na zaidi ya yote huduma hii ni bure kabisa kwa wananchi, hakuna malipo yoyote," alisisitiza Mhe. Mkude.

Kwa upande wake Naibu Mstahiki Meya Mhe. Ester Makune alisema kuwa, Manispaa ya Shinyanga katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani imeamua kutoa Mitungi hiyo 39 ya Gesi kwa wawakilishi wa wanawake wajasiriamali wawili kutoka katika kila Kata, hatua hiyo inafuatia juhudi zao katika ujasiriamali wanaoendelea nao katika kukuza kipato cha familia na Taifa kwa ujumla.

Naibu Mtahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mh. Ester Makune, akizungumza kwenye mkutano.

Katika hatua nyingine hadhara hiyo ilitumia muda huo kufanya Harambee ya Ujenzi wa Bweni la wanafunzi katika Shule ya Sekondari Mwamashele, ambapo Manispaa ya Shinyanga ilichangia kiasi cha Tzs 500,000/= Taslimu ikiwa ni mchango wao.

Siku ya Wanawake Duniani ilianza kuadhimishwa rasmi duniani mwaka 1975 ambapo Umoja wa Mataifa ulitangaza rasmi siku hiyo kuwa ni Siku ya Wanawake Duniani ambapo Tanzania ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa inasherehekea kama Nchi nyingine Duniani.

Tangazo

  • UANDIKISHWAJI WA WANAFUNZI DARASA LA AWALI NA LA KWANZA January 06, 2023
  • TANGAZO LA KAZI YA SENSA May 05, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA MPYA June 20, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA KUSIMAMIA UCHAGUZI WA MADIWANI KATA YA MWAMALILI December 07, 2022
  • Tazama

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI

    March 25, 2023
  • KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MRADI WA BARABARA INAYOJENGWA NA WALENGWA WA TASAF MANISPAA SHINYANGA

    March 16, 2023
  • RC MNDEME AZURU SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, AAGIZA SPIDI YA UJENZI KUONGEZEKA

    March 16, 2023
  • MANISPAA YA SHINYANGA YAKABIDHI PIKIPIKI MOJA KWA MTENDAJI KATA WA KATA YA MWAWAZA

    March 12, 2023
  • Tazama

Video

MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU SHINYANGA MC
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0767042958

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga