• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

SHINYANGA YAADHIMISHA MIAKA 61 YA UHURU, WANANCHI WAASWA KUONDOKANA NA UMIMI

Posted on: December 9th, 2022

Na George Mganga, Shinyanga Manispaa

NAIBU Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Utaribu). Bw. Kaspar Kaspar Mmuya, amewataka wananchi wa Shinyanga kuhakikisha wanaondoa umimi katika kutekeleza majukumu yao ili kulisaidia Taifa kuzidi kusonga mbele kimaendeleo.

Hayo ameyasema Disemba 9, 2022 katika Maadhimisho ya Uhuru wa miaka 61 Tanzania ambayo yalifanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM) ambapo kulifanya mdahalo huku mgeni rasmi akiwa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga, Prof. Siza D. Tumbo.

Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Utaribu). Bw. Kaspar Kaspar Mmuya, akizungumza katika mdahalo wa Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru.

Akizungumza na Watumishi mbalimbali wa serikali, Kamati ya Ulinzi na Usalama, viongozi wastaafu, na wananchi waliojitokeza katika ukumbi huo kwa ajili ya mdahalo uliokumbushia zaidi historia ya taifa na maoni mbalimbali kuhusu maendeleo ya nchi, Mmuya ametoa rai akieleza italisaidia taifa kufika mbali kimaendeleo kuliko kuwekeza nguvu za ubinafsi.

“Naombeni nafasi zetu tulizonazo tuzitumie zaidi katika kuleta maendeleo ya taifa, tuache kuwa na umimi ambao hauwezi kutupeleka popote kimaendeleo.

“Tumekuwa na umimi zaidi, tumeacha kulifikiria taifa letu na badala yake tunajifikiria zaidi wenyewe kitu ambacho hakitaweza kustawisha maendeleo yetu. Tulenge mbele zaidi”, alisema.

Katika hatua nyingine Mmuya amewaomba watanzania kuwalea watoto katika malezi yaliyo bora akieleza kuwa kwa sasa kumekuwa na changamoto katika eneo hilo.

Mmuya ameeleza kizazi cha sasa kimekuwa na malezi ambayo yamekuwa ni changamoto kwa kizazi kijacho na akibainisha ili kuepukana na hayo ni vizuri kuwalea katika mazingira ambayo wazee walipitia.

“Tuliangalie eneo la malezi, kumekuwa na changamoto kubwa ambayo inabidi ifanyiwe kazi. Tuwalee watoto wetu katika mazingira ambayo yatawasaidia kuja kuwa na mchango mzuri katika taifa letu”, alisema.

Mbali na malezi, Mmuya amewashauri pia vijana kuacha kulalamika kuwa hakuna kazi na badala yake watumie fursa mbalimbali zilizopo kuzifanyia kazi ikiwemo fursa za kilimo na ufugaji kwa kuwa zinachangia zaidi katika kustawisha maendeleo.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Mh. Elias Masumbuko alitumia nafasi ya mdahalo huo kupitia historia iliyotolewa na wazee ambao ni wastaafu kukumbuka nchi ilipotoka.

“Tuangalie tulipotoka, utamaduni tunaoishi nao siyo mbaya. Tutambue kuwa hapa tulipofika ni kutokana na jitihada za wazee wetu nasi wananchi kwa ujumla kwa kushirikiana na serikali.

“Nchi hujengwa kwa hekima pia busara, tulinde tunu za taifa na tusherehekee madhimisho ya uhuru wa taifa letu kwa amani”, alisema Mh. Masumbuko.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mh. Elias Masumbuko akizungumza katika mdahalo.

Katika maadhimisho hayo ya miaka 61 ya Uhuru, Katibu Tawala aligawa vyeti vya pongezi kwa Shule za Sekondari za Ngokolo na Uhuru zilizoshiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu na wa pete kama sehemu ya kutambua maendeleo ya taifa lilipotoka na lilipo kwa sasa.

Watu mbalimbali ikiwemo Kamati ya Usalama waliojitokeza kwenye mdahalo wa maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru.

Vilevile, Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imeadhimisha miaka 61 ya Uhuru kwa kushiriki shughuli za kupata miti katika kambi ya wazee Kolandoto pamoja na kufanya usafi pia kushiriki kwenye tamasha la michezo lililokutanisha shule za Ngokolo na Uhuru.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga