• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MAFUNZO YA WAFUGAJI YATOLEWA MANISPAA YA SHINYANGA

Posted on: September 2nd, 2023

Mafunzo ya namna bora ya ufugaji wa ng’ombe yametolewa jana tarehe 01-09-2023 na wataalamu wa mifugo kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, kwa hisani ya Mama O Dairies ambaye ndiye mfadhili mkuu wa Mafunzo hayo.

Akiongea katika Mafunzo hayo, Mjasiriamali na mmiliki wa kiwanda cha uzalishaji wa Maziwa cha Mama O Dairies Kilichopo Manispaa ya Shinyanga, aliwataka wafugaji kufanya ufugaji wenye tija kwa ajili ya ukuzaji wa kipato binafsi na Taifa kwa ujumla kwa kuzingatia usafi na afya ya wateja wao.

Kutokana na uzoefu wa ufugaji kwa muda mrefu ambao umemletea mafanikio, ameona ni vema ashirikishe wafugaji wenzake wa Manispaa ya Shinyanga kwa kualika wataalamu ili wawezeshwe kupata kile kilicho bora kwa manufaa yao.

Aidha wataalamu waliwasilisha mada mbalimbali kama vile namna ya utengenezaji wa chakula cha mifugo, namna bora ya ukamuaji wa maziwa, namna bora ya kukinga mifugo na magonjwa yanayoweza kusababisha vifo, namna ya kufanya mifugo ibaki kuwa na afya na kutoa maziwa kwa wingi pamoja na uhamilishaji.

Mada hizo ziliwasilishwa na wawezeshaji, ambao ni Chrispacy Kasimbazi – Afisa Mifugo wa Manispaa, Martin L. Elias – Daktari wa Mifugo Pamoja na Alex A. Kahama – Daktari wa Mifugo

Katika kikao hicho wafugaji walipata wasaha wa kutoa Mawazo, ushauri na maombi kwa uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga hasa katika kutengewa maeneo kwa ajili ya malisho ya mifugo yao.

Mwisho kabisa Mama O aliahidi kutoa ofa ya kufanya UHAMILISHAJI kwa wafugaji 150 bure. Uhamilishaji ni kitendo cha uzalishaji wa wanyama kwa njia ya kisasa kwa kutumia mbegu za madume bora ili kupata kizazi cha wanyama bora.

Hiyo ni fursa adimu sana. Kama wewe ni mfugaji jitahidi uwe wa kwanza kupata huduma hii kwa sababu ni huduma yenye gharama kubwa lakini imekuja kwako bure kabisa.


MATUKIO KATIKA PICHA

Mwezeshaji akitoa elimu kwa wafugaji

Washiriki wakisikiliza kwa Makini



Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga