• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

JIEPUSHENI NA MIKOPO KAUSHA DAMU “ RC MNDEME.

Posted on: March 8th, 2024

“JIEPUSHENI NA MIKOPO KAUSHA DAMU “ RC MNDEME


Na. Shinyanga Mc


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amewataka wanawake wa mkoa wa shinyanga kujiepusha na mikopo ya kausha damu kwani inachangia kurudisha nyuma katika kujikwamua kiumchumi.


Mhe. Mndeme amezungumza hayo leo tarehe 8 March, 2024 katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambapo kimkoa kwa Shinyanga yamefanyika katika Viwanja vya Sabasaba kambarage katika Manispaa ya Shinyanga na kuwataka Wanawake mkoani humo wawe wavumilivu katika kipindi hiki cha mpito, ambapo Serikali inaendelea kufanya maboresho juu ya utoaji wa mikopo ya asilimia 10 na wasijiingize kwenye mikopo kausha damu.


“Mnamo mwezi Aprili 2023 Serikali ilisitisha utoaji wa mikopo asilimia 10 ya Mapato ya ndani ya halmashauri kwa makundi ya Wanawake,Vijana na watu wenye ulemavu, na ilisitisha kwa lengo Mahususi la kuboresha utoaji wa mikopo hii, na pia kufuatilia marejesho ya mikopo ili kuhakikisha mzunguko unakuwa endelevu,” amesema Mhe. Mndeme


Aidha, Mhe. Mndeme ametoa Maagizo kwa Wakuu wa Wilaya Mkoani humo, kwamba wasimamie uanzishaji wa Majukwa ya Wanawake Kiuchumi kuanzia ngazi ya Kata, sababu yanawaimarisha wanawake na kuwapa nguvu pamoja na kuinuka kiuchumi.


Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa, amempongeza Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwa amini Wanawake na kuwapatia fursa mbalimbali za uongozi, na wamewakuwa wakifanya vizuri kwa kuiga uongozi wake na kuwatumikia wananchi katika kuleta Maendeleo.


Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Shinyanga Ndg. Grace Bizulu, amewataka wanawake kuendelea kujitambua na kujiheshimu kwa kuendelea kuwalea watoto katika maadili mema huku akimshukuru Rais kwa kuwekeza katika elimu na kuwaomba wanawake kuendelea kuwahimiza watoto kupenda shule na kila mmoja kwa nafasi yake asimame katika kupiga ukatili wa kijinsia.


Kila ifikapo tarehe 8 March wanawake wote duniani husherekea siku ya wanawake duniani ambapo kwa mwaka huu 2024 Kauli mbiu inasema “Wekeza kwa Wanawake,Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii,”

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga