• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Shinyanga Municipal Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Core values
    • Strategies
  • Administration
    • Administration Boundary
    • Organization Structure
    • Departments
      • Human resource
      • Secondary Education
      • Primary School
      • Finance
      • Works
      • Agriculture and Cooperative
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Hearth
      • Cleaning and Environment
      • Land and Natural Resources
    • Units
      • Information, Communication, Technology and Public Relations
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Election
      • Procurement Management
      • Beekeeping and Forest
  • Investment Opportunities
    • Industrialization
    • Farming Opportunity
    • Livestock Keeping
    • Fish breeding
    • Education Opportunity
    • Health Opportunity
  • Our Service
    • Health services
    • Education services
    • Water Services
    • Agriculture Services
    • Livestock Services
    • Fish breeding
    • Huduma za Watumishi
    • Loans Services
    • Service to rent business rooms
    • Sewage Sanitation Services
    • Business Services
      • Business License
      • Business education
      • Industrial auditing
      • Market Managent
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Councilors
    • List of councilors
    • Committees
      • Finance and Administration Committee
      • Economics, Health and Education Committee
      • Infrastructure Committee
      • Control Aids Committee
      • Ethics Committee
    • Committees Timetable
  • Projects
    • Approved projects
    • On Progress Projects
    • Complete Projects
  • Publications
    • Municipal Bylaws
    • Customer service agreement
    • Strategic plan
    • Reports
    • Application Forms
    • Guidelines
    • Newsletter
  • Media Center
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • Video
    • Training

ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI WA TABORA YAKAMILIKA NDANI YA MANISPAA YA SHINYANGA

Posted on: February 4th, 2022

Ziara ya siku mbili kwa Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Tabora imekamilika leo katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kutembea na kujifunza katika shughuli za uendeshaji wa miradi midogo na ya kati iliyopo katika eneo la Viwandani, uanzishwaji na utunzaji wa dampo lililopo Kizumbi uanzishwaji na uendeshwaji wa machinjio ya kisasa Ndembezi.

Akitoa salamu na ujumbe kutoka Manispaa ya Tabora, kaimu Mkurugenzi ndg Gudu Malulu aliwaeleza wenyeji kuwa lengo la kusafiri kwenda Shinyanga ni kujifunza namna ambavyo wamefanikiwa mambo mbalimbali kama yalivyotajwa hapo juu.

” Kwa dhati kabisa tumedhamiria kuja kujifunza na kuchukua yale yote yenye tija kubwa yatokanayo na ziara hii ili yaende kuwa msaada mkubwa kwa Manispaa yetu ya Tabora kwa muktadha wa kuipaisha Kiuchumi, kuboresha huduma za jamii, kuongeza na kuimarisha mapato na kimaendeleo kwa ujumla ili kufikia malengo ambayo Manispaa imejiwekea hasa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023”, alisema Malulu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg Jomaary Mrisho Satura alisema kuwa ni faraja sana kwa Wana Shinyanga kwa kutembelewa na ugeni kama huo muhimu jambo bora zaidi wenye lengo la kuja kujifunza mambo ambayo wameyaona ni mema kwao na yanapatika katika Manispaa ya Shinyanga, na kwamba aliwaahidi ushirikiano wa kutosha zaidi ili waridhike na wapate walichokusudia na kiende kuwa na matokeo chanya kwa wananchi wao.

Satura alisema kwamba Shinyanga siyo bora zaidi kuliko Halmashauri zingine, lakini kitendo cha Manispaa ya Tabora kuichagua Shinyanga ni jambo jema na lenye kuleta faraja kubwa sana, na kwamba Manispaa ya Shinyanga itakwenda kujifunza pia mambo mazuri kutoka Manispaa ya Tabora.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe Elias Masumbuko, aliwashukuru sana Waheshimiwa Madiwani Kutoka Manispaa ya Tabora kwa kuiona Shinyanga na hata wakaamua kwenda kujifunza, hivyo akawaomba kuwa huru kuuliza, kuhoji, kukosoa na kuboresha pale ambapo wanaona panafaa kwa kusudi la kuleta tija na kuwahudumia wananchi wa Manispaa ya Shinyanga.

“Siyo kwamba tuu mmekuja kujifunza kutoka kwetu, hapana nasi pia kupitia ujio wenu tutajifunza mambo mengi yaliyo mazuri zaidi ambayo mmekuja nayio na huenda sisi hatukuwa nayo pia, ndiyo maana nasema mkosoe, mshauri na mhoji kwa kadiri mtavyoona ili nasi tujikosoe pia,” alisema Meya Masumbuko.

Akifunga ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora, Mhe. Ramadhani Kapela aliwashukuru sana wana Shinyanga kwa ukarimu wao waliowapatia tangu kufika kwao hapo, ushirikiano waliowapatia kwenye ziara hiyo ya kujifunza mambo mbalimbali na kwamba akiwaahidi wajumbe wote kuwa watakwenda kuyafanyia kazi yote yale waliyojifunza ili yakalete mabadiliko chanya zaidi kwa wananchi wa Manispaa ya Tabora.

Kukamilika kwa ziara hiyo ya siku mbili katika Manispaa ya Shinyanga, kunatoa fursa sasa kwa wao Waheshimiwa Madiwani kwenda kuyachakata na kuyabadilisha yale yote waliyojifunza na kuyaona kwenye ziara hiyo ili yakaonekane kwenye madiliko ya vitendo na maisha ya wananchi wao wanaowaongoza kwenye maeneo yao, sambamba na kukuza pato la Manispaa, kuboresha huduma kwa jamii, kuibua na kusimamia miradi yao wenyewe.


Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndg Gudu Malulu (wa kwanza kushoto) akitoa salamu na ujumbe kutoka Manispaa ya Tabora wakati wa utambulisho kwenye ukumbi wa Mikutano Manispaa ya Shinyanga.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg Jomaary Satura (wa kwanza kushoto) akielezea jambo mbele ya wajumbe kabla ya kuanza ziara hawapo pichani.


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela akiwashukuru Waheshimiwa Madiwani wa Shinyanga, Menejimenti na wote walioshiriki kukamisha ziara hiyo.


Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • View

Latest News

  • RC MHITA AKABIDHIWA RASMI OFISI YA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA

    July 01, 2025
  • BOTI MPYA YA UOKOAJI ZIWA VICTORIA YAWASILI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 25, 2025
  • MANISPAA YA SHINYANGA YASAINI MIKATABA YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA MIJI TANZANIA.

    June 25, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI

    June 24, 2025
  • View

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
More Videos

Quick Links

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Varios Report
  • Council bylaws

Related Links

  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • President's Office Public Service Management
  • Ministry of Education,Science and Technology
  • The National Examinations Council of Tanzania
  • Shinyanga Region
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Tanesco S, Mwanza Road

    Postal Address: P.O.Box 28 Shinyanga

    Telephone: +255-28-2763213

    Mobile: 0759 023 788

    Email: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sitemap
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Copyright ©2018 Shinyanga Municipal Council . All rights reserved.