• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Shinyanga Municipal Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Core values
    • Strategies
  • Administration
    • Administration Boundary
    • Organization Structure
    • Departments
      • Human resource
      • Secondary Education
      • Primary School
      • Finance
      • Works
      • Agriculture and Cooperative
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Hearth
      • Cleaning and Environment
      • Land and Natural Resources
    • Units
      • Information, Communication, Technology and Public Relations
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Election
      • Procurement Management
      • Beekeeping and Forest
  • Investment Opportunities
    • Industrialization
    • Farming Opportunity
    • Livestock Keeping
    • Fish breeding
    • Education Opportunity
    • Health Opportunity
  • Our Service
    • Health services
    • Education services
    • Water Services
    • Agriculture Services
    • Livestock Services
    • Fish breeding
    • Huduma za Watumishi
    • Loans Services
    • Service to rent business rooms
    • Sewage Sanitation Services
    • Business Services
      • Business License
      • Business education
      • Industrial auditing
      • Market Managent
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Councilors
    • List of councilors
    • Committees
      • Finance and Administration Committee
      • Economics, Health and Education Committee
      • Infrastructure Committee
      • Control Aids Committee
      • Ethics Committee
    • Committees Timetable
  • Projects
    • Approved projects
    • On Progress Projects
    • Complete Projects
  • Publications
    • Municipal Bylaws
    • Customer service agreement
    • Strategic plan
    • Reports
    • Application Forms
    • Guidelines
    • Newsletter
  • Media Center
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • Video
    • Training

Watumishi wa Umma Hatuwezi kwenda mbele bila kubadilika kiakili

Posted on: June 23rd, 2017

Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga ndugu Albert G. Msovela ametoa wito wa kufanya kazi kwa bidii kwa watumishi wa Halmashauri ya Manispaa Shinyanga ili kumuwakilisha vizuri Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli katika kutoa huduma bora kwa wananchi. Alitoa wito huo katika ukumbi wa mikutano wa Lewis Kalinjuna uliopo ofisi za Manispaa katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2017 ambayo ilianza tarehe 16 Juni 2017.

Aidha Katibu Tawala amewaambia watumishi wa Umma waendelee kufanya kazi kwa uwazi na kwa weredi ili wanapoelekea mwisho wa mwaka 2016/2017 waweze kufanya tathimini ya mipango iliyopangwa mwanzoni mwa mwaka. Ameeleza kuwa urasimu, matumizi mabaya ya madaraka, majungu kazini, mijadala na maneno yasiyo na tija yasiwepo katika utendaji kazi.

“Tusipoyatekeleza haya, hata majukumu yako haya hutaweza kuyatekeleza. Lazima mtumishi wa Umma utambue sheria, kanuni  na miongozo ya utumishi wa umma inasemaje, tuko kwenye mamlaka ya Serikali za Mitaa, nini wajibu wetu?. Kuna matatizo mengi yametupata kutokana na kutokuzingatia kanuni, sheria na miongozo ya utumishi wa umma. Kwa hiyo niwaombe ndungu zangu watumishi tuzingatie sheria, kanuni na miongozo iliyopo katika utumishi wa umma”. Alisema Katibu Tawala Mkoa.

Mkurugenzi wa Manispaa-Geoffrey Mwangulumbi akizungumza na watumishi wa Manispaa.  

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ndugu Geoffrey Ramadhan Mwangulumbi mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa watumishi wa Manispaa amezungumza na watumishi wa Manispaa kwa kusikiliza na kujibu maswali mbalimbali ya watumishi wa umma akishirikiana na wakuu wa Idara mbalimbali. Pia ametumia mkutano huo kuwaelimisha watumishi wa umma sera, sheria, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma. Mkutano wa watumishi ulijumuisha makundi mbalimbali ya watumishi waliopo katika Halmashauri ya Manispaa wakiwemo Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule, Watumishi wote waliopo makao Makuu ya Halmashauri na Idara ya Afya, na Wakuu wa Vituo vya Afya.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma imekuwa na ujumbe wa “Ushirikishwaji wa Jamii-Vijana washirikishwe katika masuala ya kijamii barani Afrika” ambapo Manispaa ya Shinyanga iliongeza muda wa saa moja zaidi kila siku ili kutoa fursa zaidi ya kutoa huduma bora kwa wananchi. Sambamba na uongezaji wa muda wa kuhudumia wananchi, pia ofisi ya Manispaa ilijenga banda huru la kutoa elimu ya utumishi wa Umma katika viwanja vya Zimamoto, na kusikiliza maoni ya wananchi katika sehemu zinapotolewa huduma za maji katika kijiji cha Mwamagunguli na Mwamalili, kero za ardhi zilisikilizwa katika kijiji cha Nhelegani.

Watumishi wa Manispaa wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa katika kilele cha Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma


Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • View

Latest News

  • RC MHITA AKABIDHIWA RASMI OFISI YA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA

    July 01, 2025
  • BOTI MPYA YA UOKOAJI ZIWA VICTORIA YAWASILI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 25, 2025
  • MANISPAA YA SHINYANGA YASAINI MIKATABA YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA MIJI TANZANIA.

    June 25, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI

    June 24, 2025
  • View

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
More Videos

Quick Links

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Varios Report
  • Council bylaws

Related Links

  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • President's Office Public Service Management
  • Ministry of Education,Science and Technology
  • The National Examinations Council of Tanzania
  • Shinyanga Region
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Tanesco S, Mwanza Road

    Postal Address: P.O.Box 28 Shinyanga

    Telephone: +255-28-2763213

    Mobile: 0759 023 788

    Email: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sitemap
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Copyright ©2018 Shinyanga Municipal Council . All rights reserved.