- Home
- About Us
- Administration
- Investment Opportunities
- Our Service
- Councilors
- Projects
- Publications
- Media Center
MWL.KAGUNZE AKAGUA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI NGOKOLO B
Na.Shinyanga Mc
Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Mwl. Alexius Kagunze leo tarehe 2 Oktoba, 2023 amekagua Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Ngokolo B inayojengwa katika Kata ya Ndembezi Mtaa wa Butengwa.
Mwl. kagunze amekagua ujenzi huu ambao ulianza rasmi mwezi Septemba na kuridhishwa na kasi ya ujenzi unaoendelea na kuwataka mafundi wasipunguze kasi ya ujenzi na kuwataka wajenge kwa kuzingatia viwango vya kulingana na thamani ya fedha iliyotolewa na Serikali.
"Nimefurahishwa na kasi ya ujenzi unaoendelea niwaombe msipunguze kasi ili ifikapo mwezi Desemba, 2023 ujenzi umekamiliki ili mwakani tuweze kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza" alisema Mwl. Kagunze
Shule Mpya ya Ngokolo B Sekondari, Manispaa ya Shinyanga ilipokea kiasi cha Tsh Milioni 603,890,200/= kutoka Serikali kuu ambapo itatumika kujenga Madarasa 8, Jengo la Utawala 1, Matundu ya Vyoo 22, Jengo la Tehama 1,Maktaba 1 na Maabara 3.
Kukamilika kwa ujenzi huu wa Shule utasaidia kupunguza Msongamano kwa wanafunzi wanaojazana kwa wingi katika shule ya Sekondari Ngokolo ambapo wengi huchaguliwa katika shule hiyo.
Shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia suluhu Hassan kwa kuendelea kuwezesha Sekta zote hususani Sekta ya elimu Manispaa ya Shinyanga.MWL.
Tanesco S, Mwanza Road
Postal Address: P.O.Box 28 Shinyanga
Telephone: +255-28-2763213
Mobile: 0759 023 788
Email: md@shinyangamc.go.tz
Copyright ©2018 Shinyanga Municipal Council . All rights reserved.