• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Shinyanga Municipal Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Core values
    • Strategies
  • Administration
    • Administration Boundary
    • Organization Structure
    • Departments
      • Human resource
      • Secondary Education
      • Primary School
      • Finance
      • Works
      • Agriculture and Cooperative
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Hearth
      • Cleaning and Environment
      • Land and Natural Resources
    • Units
      • Information, Communication, Technology and Public Relations
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Election
      • Procurement Management
      • Beekeeping and Forest
  • Investment Opportunities
    • Industrialization
    • Farming Opportunity
    • Livestock Keeping
    • Fish breeding
    • Education Opportunity
    • Health Opportunity
  • Our Service
    • Health services
    • Education services
    • Water Services
    • Agriculture Services
    • Livestock Services
    • Fish breeding
    • Huduma za Watumishi
    • Loans Services
    • Service to rent business rooms
    • Sewage Sanitation Services
    • Business Services
      • Business License
      • Business education
      • Industrial auditing
      • Market Managent
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Councilors
    • List of councilors
    • Committees
      • Finance and Administration Committee
      • Economics, Health and Education Committee
      • Infrastructure Committee
      • Control Aids Committee
      • Ethics Committee
    • Committees Timetable
  • Projects
    • Approved projects
    • On Progress Projects
    • Complete Projects
  • Publications
    • Municipal Bylaws
    • Customer service agreement
    • Strategic plan
    • Reports
    • Application Forms
    • Guidelines
    • Newsletter
  • Media Center
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • Video
    • Training

MIAKA MIWILI YA MH DKT. SAMIA SHINYANGA YAKUSANYA BIL 255 ZA MADINI

Posted on: March 25th, 2023

MKOA wa Shinyanga umekusanya zaidi ya shilingi Bilioni 255 kama mapato yatokanayo na shughuli za Madini, katika kipindi cha miaka miwili ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan madarakani.

Hayo yamebainishwa leo Machi 25, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mh. Christina Mndeme katika Kongamano la miaka miwili ya mafanikio ya Utawala wa Rais Samia lililofanyika leo Machi 25, 2023 katika ukumbi wa Mikutano wa Jengo la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali, wakiwamo na Wabunge wa Mkoa wa Shinyanga.

Mh. Mndeme ameeleza kuwa Makusanyo hayo yanahusisha ada za leseni, mrabaha na ada za ukaguzi zinazokusanywa kupitia Wizara ya Madini.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Shinyanga umetoa leseni mbalimbali za madini 827 katika kipindi hicho cha miaka miwili.

Ameongeza kuwa vituo viwili vya ununuzi wa madini vimeanzishwa ikiwa ni mkakati wa kusogeza huduma za biashara ya madini karibu na maeneo ya wachimbaji wadogo.

Mndeme ametoa taarifa hiyo wakati wa kongamano la kuangazia mafanikio yaliyopatikana mkoani Shinyanga ndani ya kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika hatua nyingine, Mh. Mndeme amesema Mkoa wa Shinyanga umefanikiwa kujenga vyumba vipya vya madarasa 833, mabweni 3 na matundu ya vyoo 1,003 katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akielezea mafanikio ya miaka miwili ya Rais Samia.

Amesema “Mkoa umepokea zaidi ya shilingi Bilioni 37.68 katika sekta ya elimu na kufanikiwa pia kukarabati shule kongwe mbili za msingi”.

Amesema zaidi ya shilingi Bilioni 3.18 zimetumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa 108, mabweni 3, matundu ya vyoo 1,002 na kukarabati shule kongwe mbili za msingi.

Amesema “shilingi Biliioni 20.32 zimetuika kujenga shule mpya 7, vyumba vya madarasa 725 kwa shule za sekondari, shilingi bilioni 11.96 zimetumika kugharamia elimu bila ada na shilingi bilioni 2.21 zimetumika katika ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Wilayani Kishapu”.

Aidha, katika Utawala wa miaka miwili ya Rais, Dkt. Samia, Mh. Mndeme amesema Mkoa wa Shinyanga umejenga viwanda vipya 108 katika kipindi cha miaka miwili kuanzia mwezi Machi mwaka 2021 hadi mwezi Februari mwaka huu  na kuufanya kufikisha jumla ya viwanda 838.

Kabla ya kujengwa kwa viwanda hivyo vipya, mkoa huo ulikuwa na viwanda 730, lakini kutokana na fursa za uwekezaji zilizofunguliwa na Serikali ya awamu ya sita viwanda 108 zaidi vimejengwa katika mkoa huo ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.79.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi akielezea mafanikio ya miaka miwili ya Rais Samia katika Wilaya ya Shinyanga.

Viwanda vingi ni vile vinavyoongeza thamani ya mazao ya kilimo na mifugo pamoja na uchimbaji wa madini ya dhahabu na almasi.

Mbali na Mh. Mdeme, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mh. Johari Samizi, amebainisha kuwa katika Utawala wa Miaka miwili ya Mama Samia, ndani ya Wilaya ya Shinyanga, Miradi ya Ujenzi wa Masoko ikiwemo Soko la Ibinzamata, Ngokolo Mtumbani na Soko Kuu inayotekelezwa na Mapato ya Ndani kutoka Halmashauri ya manispaa ya Shinyanga inaendelea, halikadhalika Ujenzi wa Vituo vya Afya ikiwamo Ihapa na Kambarage ambayo Serikali imewezesha kujenga ili kuongeza ufanisi wa huduma.

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • View

Latest News

  • RC MHITA AKABIDHIWA RASMI OFISI YA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA

    July 01, 2025
  • BOTI MPYA YA UOKOAJI ZIWA VICTORIA YAWASILI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 25, 2025
  • MANISPAA YA SHINYANGA YASAINI MIKATABA YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA MIJI TANZANIA.

    June 25, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI

    June 24, 2025
  • View

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
More Videos

Quick Links

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Varios Report
  • Council bylaws

Related Links

  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • President's Office Public Service Management
  • Ministry of Education,Science and Technology
  • The National Examinations Council of Tanzania
  • Shinyanga Region
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Tanesco S, Mwanza Road

    Postal Address: P.O.Box 28 Shinyanga

    Telephone: +255-28-2763213

    Mobile: 0759 023 788

    Email: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sitemap
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Copyright ©2018 Shinyanga Municipal Council . All rights reserved.