• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Shinyanga Municipal Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Core values
    • Strategies
  • Administration
    • Administration Boundary
    • Organization Structure
    • Departments
      • Human resource
      • Secondary Education
      • Primary School
      • Finance
      • Works
      • Agriculture and Cooperative
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Hearth
      • Cleaning and Environment
      • Land and Natural Resources
    • Units
      • Information, Communication, Technology and Public Relations
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Election
      • Procurement Management
      • Beekeeping and Forest
  • Investment Opportunities
    • Industrialization
    • Farming Opportunity
    • Livestock Keeping
    • Fish breeding
    • Education Opportunity
    • Health Opportunity
  • Our Service
    • Health services
    • Education services
    • Water Services
    • Agriculture Services
    • Livestock Services
    • Fish breeding
    • Huduma za Watumishi
    • Loans Services
    • Service to rent business rooms
    • Sewage Sanitation Services
    • Business Services
      • Business License
      • Business education
      • Industrial auditing
      • Market Managent
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Councilors
    • List of councilors
    • Committees
      • Finance and Administration Committee
      • Economics, Health and Education Committee
      • Infrastructure Committee
      • Control Aids Committee
      • Ethics Committee
    • Committees Timetable
  • Projects
    • Approved projects
    • On Progress Projects
    • Complete Projects
  • Publications
    • Municipal Bylaws
    • Customer service agreement
    • Strategic plan
    • Reports
    • Application Forms
    • Guidelines
    • Newsletter
  • Media Center
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • Video
    • Training

MANISPAA YA SHINYANGA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUGAWA MITUNGI YA GESI 39

Posted on: March 10th, 2023

HALMASHAURI ya Manispaa ya Shinyanga ni miongoni mwa Halmashauri Nchini iliyoshiriki kikamilifu katika kuadhimisha kilele cha Sherehe za Siku ya Wanawake Duniani ambayo Kimkoa ilifanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Machi 8, 2023.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi 39.

Akizungumza wakati wa Sherehe hizo, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, aliseama kuwa wanawake ni kundi kubwa lenye nguvu zaidi katika nyanja mbalimbali ikiwamo Uongozi, Uchumi, Kijamii na kadhalika hivyo katika kuadhimisha siku yao ni muhimu sana wakapongezwa na kupewa nguvu zaidi ili wakaongeze jitihada.

Hivyo basi katika kuhakikisha kuwa Serikali inawajali na kuwaongezea nguvu kwa kuwapatia mitungi ya Gesi bure kabisa jambo ambalo litaenda kuboresha na kuongeza tija kwa shughuli zao za kila siku katika kujipatia kipato cha familia zao na Taifa pia, kwani wataondokana na matumizi ya mkaa au kuni jambo ambalo linatumia muda mrefu zaidi katika kupika kulinganisha na matumizi ya Gesi.

“Ukitazama hasa katika kipindi hiki Wanawake wamekuwa na mchango mkubwa sana katika jamii zetu na Nchi kwa ujumla kama ambavyo unamuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi bora zaidi, kuna Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Tulia Akson anaongoza vema kabisa Bunge letu na wengine wengi zaidi Tanzania na nje ya Nchi hii ni kielelezo kuwa wanawake ni kundi kubwa na muhimu zaidi.

"Kwa msingi huu sasa nawapongeza sana Manispaa ya Shinyanga kwa kuamua kuwapatia mitungi ya gesi bure kwa wanawake wajasiriamali wao kutoka katika Kata zao zote 17 za Manispaa, jambo ambalo ni la kuigwa na Halmashauri nyingine kwani watakuwa wanakwenda na Kauli Mbiu isemayo Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia, Chachu katika kuleta Usawa wa Kijinsia maana yake Manispaa wamekuwa wabunifu na kuwaletea mabadilko wajasiriamali wao ambayo ni chachu kwao " alisema Mhe. Mkude.

Mhe. Mkude aliwakumbusha pia wananchi wote waliofika katika sherehe hiyo juu ya umuhimu wa kuchukua tahadhari zaidi kwa ugonjwa wa Homa Kali na Joto yaani UVIKO 19 kwani ugonjwa huo upo na kwamba kwa wale ambao hawajamalizia Chanjo ya pili wafanye hivyo haraka kutoka na umuhimu wake.

"Tuendelee kuchukua tahadhari zaidi kwa ugonjwa huu, na ikumbukwe kwamba hakuna madhara yoyote kwenye Chanjo hizo zinazotolewa na Serikali kupitia Sekta ya Afya katika vituo vyote vya Afya na zaidi ya yote huduma hii ni bure kabisa kwa wananchi, hakuna malipo yoyote," alisisitiza Mhe. Mkude.

Kwa upande wake Naibu Mstahiki Meya Mhe. Ester Makune alisema kuwa, Manispaa ya Shinyanga katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani imeamua kutoa Mitungi hiyo 39 ya Gesi kwa wawakilishi wa wanawake wajasiriamali wawili kutoka katika kila Kata, hatua hiyo inafuatia juhudi zao katika ujasiriamali wanaoendelea nao katika kukuza kipato cha familia na Taifa kwa ujumla.

Naibu Mtahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mh. Ester Makune, akizungumza kwenye mkutano.

Katika hatua nyingine hadhara hiyo ilitumia muda huo kufanya Harambee ya Ujenzi wa Bweni la wanafunzi katika Shule ya Sekondari Mwamashele, ambapo Manispaa ya Shinyanga ilichangia kiasi cha Tzs 500,000/= Taslimu ikiwa ni mchango wao.

Siku ya Wanawake Duniani ilianza kuadhimishwa rasmi duniani mwaka 1975 ambapo Umoja wa Mataifa ulitangaza rasmi siku hiyo kuwa ni Siku ya Wanawake Duniani ambapo Tanzania ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa inasherehekea kama Nchi nyingine Duniani.

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • View

Latest News

  • RC MHITA AKABIDHIWA RASMI OFISI YA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA

    July 01, 2025
  • BOTI MPYA YA UOKOAJI ZIWA VICTORIA YAWASILI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 25, 2025
  • MANISPAA YA SHINYANGA YASAINI MIKATABA YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA MIJI TANZANIA.

    June 25, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI

    June 24, 2025
  • View

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
More Videos

Quick Links

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Varios Report
  • Council bylaws

Related Links

  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • President's Office Public Service Management
  • Ministry of Education,Science and Technology
  • The National Examinations Council of Tanzania
  • Shinyanga Region
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Tanesco S, Mwanza Road

    Postal Address: P.O.Box 28 Shinyanga

    Telephone: +255-28-2763213

    Mobile: 0759 023 788

    Email: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sitemap
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Copyright ©2018 Shinyanga Municipal Council . All rights reserved.