• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

Waganga Wakuu waaigizwa kila Hospitali kuwa na Dawa za Wazee

Posted on: July 26th, 2017

Waganga Wakuu wa Mikoa yote wameagizwa kuhakikisha kila Hopitali inakuwa na dawa maalumu kwa ajili ya wazee pamoja na kuwabaini wazee wote katika mikoa yao ili wapate huduma za afya bila malipo. Naibu Waziri wa Afya Dkt. Hamis Kigwangala ametoa agizo hilo alipotembelea kituo cha Wazee cha Kolandoto kilichopo katika Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga. "Hakuna maana yoyote kama mzee anapimwa na tatizo lake linafahamika halafu akifika kwenye dirisha la dawa anaambiwa dawa zimeisha hapa nenda kanunue" amesema Dkt.Kigwangala.

Dkt. Kigwangala amewahakikishia Wazee kuwa, Serikali itahakikisha kuwa hali ya upatikanaji wa huduma za jamii kama vile chakula, malazi na dawa inaimarika ikiwemo mikakati madhubuti ya kuwapatia huduma bila malipo na kuwalinda. Amesema kulingana na sensa ya mwaka 2013 idadi ya Wazee nchini ni milioni 2.5 ambayo ni sawa na asilimia 5.6 ya wananchi wote na inakadiriwa kuongezeka na kufikia wazee milioni 2.7 mwezi Desemba, 2017, hivyo Wizara ya Afya inasimamia maslahi na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi.

Awali, Mwenyekiti wa kituo cha Wazee Kolandoto Mzee Somola Maganga na Katibu wa Wazee Mkoa wa Shinyanga Mzee Sengerema wameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa jitihada kubwa ya kuwajali wazee na kutekeleza yale waliyoomba. Aidha, Wazee hao wameomba kuwa na Daktari bingwa wa magonjwa ya wazee hususani ugonjwa wa tezi dume.

Kuhusu watumishi wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Dkt. Kigwangala amesema Wizara itaendelea kushughulikia changamoto zinazowakabili ili waweze kutekeleza majukumu yao vema. Katika ziara hiyo, Naibu Waziri wa Afya ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa bweni la wazee wa kituo cha Wazee Kolandoto, bweni  litakalobeba wazee 20. Pia amefungua jiko la gesi, amekabidhi bajaji pamoja na kiboksi cha huduma ya kwanza kwa wazee hao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MHE. MWEBEA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 05, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO OPD KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUKAMILIKA

    June 03, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO LA UTAWALA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUMALIZA UJENZI

    June 02, 2025
  • WANAFUNZI KUTOKA SHULE 20 ZA MANISPAA YA SHINYANGA WAKUTANA KUBADILISHANA UJUZI ILI KUBORESHA TAALUMA.

    May 17, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga