• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

Vituo vya Kutolea Huduma kuanza kutumia mfumo wa FFARS

Posted on: June 8th, 2017

Mafunzo ya siku mbili kuhusu mfumo wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha kwa ngazi za vituo vya kutolea huduma ‘Facility Financial Accounting and Reporting System – FFARS) (FFARS) kupitia mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) na mradi wa Tuimairishe Afya-HPSS (Health Promotion and System Strengthening) yameanza  leo katika hoteli ya Vigmark mjini Shinyanga.

Zaidi ya washiriki 60 katika makundi ya waratibu elimu kata katika kata zote za Halmashauri ya Manispaa na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, mkuu wa kituo cha afya na mhasibu wa kila hospitali ya wilaya wamepatiwa mafunzo ya Mfumo wa FFARS katika vituo vya kutolea huduma zikiwemo zahanati, vituo vya afya, hospitali na shule za msingi na sekondari.

Mojawapo ya kundi la washiriki wa semina wakiwa kwenye mazoezi ya vitendo ya ujazaji wa daftari la fedha katika sekta ya afya na elimu

Mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha washiriki hao ili waweze kuufahamu mfumo na kuweza kwenda kutoa mafunzo ya utumiaji wa mfumo wa FFARS kwa watoa huduma waliopo katika ngazi za shule za msingi na sekondari, na vituo vya afya wakiwemo kila mkuu wa kituo cha afya, mhasibu wa kila shule ya msingi na sekondari.

Mafunzo ya leo ni matokeo ya mafunzo yaliyofanyika tarehe 5 hadi 6 Juni 2017 ambapo wahasibu zaidi ya 130 kutoka Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Majiji kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kati walipatiwa mafunzo ya Mfumo wa FFARS ambao kwa leo wamekuwa wawezeshaji kwa washiriki zaidi ya 60 waliohudhuria mafunzo. Wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka PS3, TAMISEMI, Wizara ya afya, HPSS (Health Promotion and System Strengthening) na Wizara ya Elimu wameshiriki katika kutoa mafunzo kwa kuhakikisha mafunzo yanaendeshwa kwa ufanisi wenye matokeo chanya.

Wakati akifungua mafunzo, mkuu wa Idara ya Ufuatiliaji, Tathmini na Tafiti Tendaji kutoka PS3, Dr. Suma Kaare, alisema mfumo wa kutumia njia za kielektroniki (kompyuta) katika kuingiza taarifa za kifedha za vituo vya kutolea huduma utasaidia kurahisisha kazi na tayari serikali imeukubali na utaanza kutumika kuanzia mwezi Julai, 2017 katika halmashauri mbalimbali.


Dr. Suma Kaare, Mkuu wa Idara ya Ufuatiliaji, Tathmini na Tafiti Tendaji kutoka PS3.Kulia ni Bi.Catherine Oyoga Mhasibu katika Mifumo ya Fedha TAMISEMI

Baada ya mafunzo haya, wahitimu wataenda kutoa mafunzo katika vituo vya kazi vinavyotoa huduma kuanzia tarehe 19 hadi 30 Juni 2017. Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ina jumla ya vituo vya Serikali 76 vinavyotoa huduma katika sekta ya Elimu na Afya ambavyo vitaanza kutumia mfumo wa FFARS kutoa taarifa za fedha. Kuna Shule za Msingi 48, shule za sekondari 17, vituo vya afya 1, zahanati 9 na Hospitali 01 yenye hadhi ya 'Council Designed Hospital' iliyopo Kolandoto. 

Bonyeza hapa kupakuwa mada zilizofundishwa kwa washiriki wa semina

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga