• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

RC MACHA AWASIHI WANANCHI KUENZI NA KUDUMISHA MUUNGANO WA TANZANIA.

Posted on: April 26th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, amewasihi wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuendelea kuenzi na kudumisha Muungano uliosimikwa na waasisi wa taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.


Mhe. Macha ametoa wito huu leo, Aprili 26, 2025, wakati akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Shinyanga katika maadhimisho ya miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaliyofanyika katika mtaa wa Mabambasi, kata ya Ndembezi. Maadhimisho hayo yameambatana na shughuli za usafi wa mazingira na upandaji miti, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhifadhi mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.


“Muungano wa Tanzania ni wa kihistoria katika bara la Afrika. Nchi kadhaa zilijaribu kuungana lakini muungano wao haukudumu. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ndio muungano wa kipekee uliojaa amani na mshikamano. Niwasihi wananchi waendelee kuuenzi Muungano huu kama ilivyokuwa dhamira ya waasisi wetu,” amesema Mhe. Macha.


Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amewasihi wakazi wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,awamu ya pili linalotarajiwa kufanyika Mei 1-7, 2025. Kwa mkoa wa Shinyanga ambapo amesema zoezi hilo ni muhimu ili kuwawezesha wananchi kutumia haki yao ya kidemokrasia kupiga kura katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2025 na kuwachagua viongozi bora wa kuliongoza taifa kwa kipindi kijacho.


Naye Mkuu wa Idara ya Maliasili na Mazingira Manispaa ya Shinyanga, Ndg. Ezra Manjerenga, ameeleza kuwa katika kuhakikisha miti inayopandwa inastawi vizuri na kuhifadhiwa, Halmashauri imekuja na kaulimbiu isemayo, “MTU NA MTI, MTI NA MTU”, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuimarisha utunzaji mazingira na kuhimiza ushiriki wa wananchi katika utunzaji wa mazingira yao.


Maadhimisho ya Miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Mwaka 2025 yanaongozwa na Kauli mbiu isemayo “Muungano Wetu ni Dhamana, Heshima na Tunu kwa Taifa: Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga