• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MKUU WA WILAYA AZINDUA KAMPENI YA UPANDAJI MITI MANISPAA YA SHINYANGA KUADHIMISHA MIAKA 60 YA UHURU

Posted on: November 26th, 2021

Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imezindua Kampeni ya upandaji wa miti ya matunda na vivuli kuelekea katika maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika, na miaka 59 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni nyenzo moja wapo ya kukabiliana na madhara yanayosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.

Uzinduzi huo umefanyika Novemba 20,2021 katika viwanja vya machinjio ya ng’ombe ya Kisasa kata ya Ndembezi ambao umeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko na kuhudhuriwa na viongozi na wakuu wa taasisi na Idara mbalimbali za serikali na zisizo za kiserikali, wadau wa maendeleo pamoja na wakazi wa manispaa ya Shinyanga, ambapo jumla ya miti 2,000 imepandwa na kugawiwa wakazi wa eneo hilo.

Akizindua kampeni hiyo Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko amewataka wananchi kuacha tabia ya kukata miti na badala yake waitunze ili kupunguza kama si kumaliza madhara yanayosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi, mfano kuongezeka kwa joto duniani.

“Tuendelee kuilinda miti tuliyoipanda kipindi cha nyuma, lakini pia tuendelee kupanda miti mipya, tuisimamie iote pamoja na kuhakikisha usalama wa miti ili mifugo isiharibu ili miti iwe imara” amesema Mboneko.

“Na safari hii Shinyanga tuna Kampeni yetu inasema Shinyanga ya miembe na mikwaju, miembe tunajua ni soko kubwa pamoja na mikwaju pia ina soko kubwa, kwa hiyo tutumie fursa hiyo ya utunzaji wa mazingira na kipato wakati mwingine, tuhakikishe tunapoadhimisha miaka 60 ya uhuru tutazame na mazingira yetu”, ameongeza Mboneko.

Mratibu wa Kampeni hiyo Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone amesema halmashauri hiyo imeweka malengo ya kupanda idadi ya miti ya matunda na vivuli milioni moja na laki tano, ambapo miti hiyo itagawiwa kwenye taasisi za umma na binafsi, shule za msingi na sekondari.

Kiwone amesema miche mingine ya miti itakabidhiwa kwa pamoja na wakazi wa manispaa ya Shinyanga ili kuunga mkono jitihada za serikali kukabiliana na ongezeko la joto duniani ambalo limesababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga Abubakar Mukadam amewataka wakazi wa Shinyanga kushirikiana na serikali katika kutatua changamoto zilizopo kwenye jamii huku akimulika suala la upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira.

“Ndugu zangu mnafahamu kila mwaka hali ya hewa inazidi kubadilika ninawaomba kuipa nguvu serikali kwa kushirikiana nayo, kila mmoja kuchukua jukumu la kupanda, kuitunza na kuisimamia miti ili kuleta unafuu wa hali ya hewa nzuri ambayo imeanza kutoweka”, amesema Mukadam.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura amewashukuru wananchi na wadau mbalimbali waliojitokeza katika upandaji miti huku akibainisha kuwa upandaji miti ni jukumu la kila mmoja katika jamii.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MHE. MWEBEA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 05, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO OPD KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUKAMILIKA

    June 03, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO LA UTAWALA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUMALIZA UJENZI

    June 02, 2025
  • WANAFUNZI KUTOKA SHULE 20 ZA MANISPAA YA SHINYANGA WAKUTANA KUBADILISHANA UJUZI ILI KUBORESHA TAALUMA.

    May 17, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga