• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MKUU WA WILAYA AFUNGUA MACHINJIO YA KISASA NDEMBEZI MANISPAA YA SHINYANGA

Posted on: November 22nd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko amezindua Machinjio ya Kisasa ya ng’ombe na mbuzi yaliyopo katika kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga huku akitoa agizo kwa Wachinjaji katika mitaa mbalimbali Mjini Shinyanga kuhamia katika machinjio hayo mapya ambayo yanafuata taratibu zote za afya.



Uzinduzi huo umefanyika leo Jumatatu Novemba 22,2021 na kuhudhuriwa na viongozi na wananchi wa Manispaa ya Shinyanga waliokuwa na kiu kubwa ya kuona machinjio hiyo inaanza kufanya kazi ili wapate fursa mbalimbali pamoja na kupata kitoweo kilichoandaliwa katika mazingira safi na salama.



“Tumezindua Machinjio haya kwa kuchinja ng’ombe wanne leo,hatukuwahi kufanya uchinjaji lakini baada ya kufanya zoezi hili tumebaini uwepo wa changamoto za kitaalamu hali inayosababisha leo zoezi litumie muda mrefu.Tutarekebisha changamoto zilizojitokeza na kesho Jumanne Novemba 23 tutaanza rasmi uchinjaji ambapo kazi itafanyika kwa kasi zaidi”,amesema Mboneko.



“Naomba tutumie machinjio haya kwani nyama inayotoka hapa itakuwa na ubora mkubwa iliyoandaliwa katika mazingira bora yanayozingatia kanuni na taratibu za afya. Machinjio zote zilizopo huko mtaani tunazifunga wiki hii ili wachinjaji wote wahamie hapa”,amesema Mboneko.



Mkuu huyo wa wilaya pia amesisitiza matumizi ya magari katika kusafirisha nyama badala ya kutumia matoroli na mifuko ili kuhakikisha nyama zinakuwa salama na bora kwa matumizi ya binadamu.



Aidha amewakaribisha wafanyabiashara wa ng’ombe na mbuzi ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kutumia machinjio hiyo kuchinja mifugo na kusafirisha nyama badala ya kusafirisha wanyama wakiwa hai.



Mboneko amewahamasisha wakazi wa eneo la Ndembezi kuchangamkia fursa zinazopatikana katika machinjio hayo ikiwemo ajira zisizo za kitaalamu huku akiwasisitiza kuwa waadilifu na waaminifu kwa kufika kazini kwa wakati na kuepuka udokozi wa nyama katika machinjio hiyo.



Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura amesema mpaka sasa mradi huo wa Machinjio ya Kisasa umegharimu zaidi ya shilingi Bilioni 5.2 huku akieleza kuwa mradi huo ulichelewa kuanza kutokana na changamoto ya Mfumo wa Majitaka na Mfumo wa Ubaridi (Cold Room) na baada ya kuzitatua uchinjaji umeanza na wanategemea kuchinja kwa kasi zaidi kuanzia kesho Jumanne.



Mwenyekiti wa Wachinjaji mkoa wa Shinyanga, Masaka Charles amesema kutokana na kuzinduliwa kwa machinjio hiyo wachinjaji wote Mjini Shinyanga watahamia hapo ili kuendesha shughuli za uchinjaji.



Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga Mhe. Abubakar Mukadam amesema machinjio hiyo imeanza kufanya kazi baada ya serikali kutatua changamoto zilizokuwepo huku akitaka siasa kutoingizwa kwenye mradi huo.



Diwani wa kata ya Ndembezi Mhe. Victor Mmanywa ameshukuru kuzinduliwa kwa machinjio hiyo ambayo itawezesha wakazi wa kata ya Ndembezi kupata fursa mbalimbali.



Nao wakazi wa Ndembezi wameeleza kufurahishwa na kuanza kazi kwa machinjio hiyo wakisema matumaini yao ni kupata fursa za ajira.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga