• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MATOKEO MAZURI DARASA LA 7, DC MTATIRO AZITUNUKU TUZO SHULE, WALIMU SHINYANGA MANISPAA

Posted on: February 17th, 2026

Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imeendelea kung’ara katika sekta ya elimu baada ya hivi karibuni kushika nafasi ya kwanza kimkoa kati ya Halmashauri sita za Mkoa wa Shinyanga katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba (PSLE) mwaka 2025, kwa kupata ufaulu wa wa jumla wa asilimia 87.


Kutokana na mafanikio hayo, Idara ya Elimu ya Awali na Msingi ya Manispaa ya Shinyanga imeandaa hafla maalum ya kutunuku vyeti vya pongezi kwa walimu pamoja na shule za msingi zilizofanya vizuri katika PSLE na Mtihani wa Upimaji wa Darasa la Nne (SFNA) kwa mwaka 2025.


Akitoa taarifa ya matokeo hayo, Mkuu wa Idara ya Elimu ya Awali na Msingi Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Mary Samson Maka, amesema kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya juhudi za pamoja kati ya walimu, wanafunzi, wazazi na wasimamizi wa elimu.


Ameongeza kuwa katika Mtihani wa Upimaji Darasa la Nne (SFNA), Manispaa ya Shinyanga imefanikiwa kushika nafasi ya kwanza kimkoa kwa kupata asilimia 82.25 ya ufaulu wa jumla, hali inayoonesha mwelekeo mzuri wa elimu ya msingi kuanzia ngazi za awali.


Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, Ndugu Revocatus Lutunda, amesema walimu ni nguzo muhimu katika maendeleo ya elimu na taifa kwa ujumla. Ametumia fursa hiyo kuwapongeza walimu kwa bidii na moyo wa kujituma, akisisitiza kuwa mafanikio hayo yanathibitisha kuwa uwekezaji katika elimu una tija kubwa.


Akikabidhi tuzo hizo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Wakili Julius Mtatiro, amewapongeza walimu pamoja na Idara ya Elimu ya Awali na Msingi kwa ubunifu wa kuwapatia motisha walimu wanaofanya vizuri huku akiwashauri walimu kujifunza kutoka kwa shule zilizofanya vizuri zaidi ili kubadilishana uzoefu, kuongeza maarifa, mbinu bora za ufundishaji na kuimarisha ubunifu katika kuinua zaidi viwango vya elimu Manispaa ya Shinyanga.


Mafanikio haya yameifanya Manispaa ya Shinyanga kuendelea kuwa mfano wa kuigwa katika sekta ya elimu, yakionesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kuboresha elimu kwa maendeleo endelevu ya jamii na taifa kwa ujumla.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MATOKEO MAZURI DARASA LA 7, DC MTATIRO AZITUNUKU TUZO SHULE, WALIMU SHINYANGA MANISPAA

    February 17, 2026
  • MANISPAA YA SHINYANGA YAENDELEA KUWAWEZESHA WALIMU WA SEKONDARI KUTEKELEZA MTAALA MPYA WA ELIMU.

    January 22, 2026
  • KAMATI YA FEDHA NA UTAWALA MANISPAAYA SHINYANGA YAWATAKA WAKANDARASI KUIPA KIPAUMBELE MIRADI YA ELIMU.

    January 21, 2026
  • WANANCHI WAASWA KUEPUKA MIKOPO KAUSHA DAMU

    January 06, 2026
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga