- Mwanzo
- Kuhusu sisi
- Utawala
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma Zetu
- Madiwani
- Miradi
- Machapisho
- Kituo cha Habari
MANISPAA YA SHINYANGA YATWAA VIKOMBE VITATU UMISSETA NGAZI YA MKOA 2025
Na: Shinyanga Mc
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imeibuka kidedea katika Mashindano ya Umoja wa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) kwa ngazi ya mkoa, baada ya kutwaa jumla ya vikombe vitatu. Manispaa hii imeshinda nafasi ya kwanza katika michezo ya Mpira wa Wavu (wavulana), Mpira wa Pete (wasichana), na Mpira wa Mezani (wasichana).
Wakikabidhi vikombe leo Juni 10, 2025 kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Mwl. Alexius Kagunze Afisa michezo manispaa ya Shinyanga Ndg. Anoldus Rukiza, Mratibu wa Michezi Manispaa ya Shinyanga Mwl. Stephano Yeyeye Pamoja na Afisa Elimu Taaluma Manispaa ya Shinyanga Mwl. Richard Makoye. Mkurugenzi wa Manispaa Mwl. Kagunze amewapongeza waratibu, wakufunzi, walimu na wanafunzi wote walioshiriki kwa bidii na kuonesha juhudi kubwa zilizowezesha ushindi huo wa kihistoria.
“Nawapongeza kwa dhati waratibu wetu wa michezo, wakufunzi, walimu na wanafunzi wote waliowakilisha Manispaa ya Shinyanga kwa mafanikio makubwa. Ushindi huu ni ushahidi wa juhudi, mshikamano na nidhamu ya hali ya juu. Tuendelee kuwekeza katika vipaji vya vijana wetu kwani michezo ni sehemu muhimu ya maendeleo ya elimu na jamii kwa ujumla,” amesema Mwl. Kagunze
Mashindano ya UMISSETA mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo:“Viongozi bora ni msingi wa maendeleo ya Taaluma, Sanaa na Michezo. Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu.” Ambapo kitaifa, yanafanyika Mkoani Iringa, yakiwakutanisha vijana wenye vipaji kutoka kila kona ya Tanzania.
Tanesco S, Mwanza Road
Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga
Simu: +255-28-2763213
Simu ya Mkononi: 0759 023 788
Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz
Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga