- Mwanzo
- Kuhusu sisi
- Utawala
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma Zetu
- Madiwani
- Miradi
- Machapisho
- Kituo cha Habari
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imeibuka mshindi wa pili kitaifa katika mashindano ya afya na usafi wa mazingira kwa mwaka 2024, ikitangazwa miongoni mwa Halmashauri za Manispaa 20 nchini, ushindi huu umeambatana na tuzo ya heshima pamoja na zawadi ya shilingi milioni 2 (Tsh 2,000,000) iliyotolewa na Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama (MB).
Tuzo hiyo ilipokelewa kwa heshima kubwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Elias R. Masumbuko, akiwa pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Usafi wa Mazingira na Udhibiti wa Taka, Ndg. Kuchibanda Snatus, hafla hiyo muhimu ilifanyika tarehe 08 Aprili 2025, mkoani Dodoma.
Ushindi huu ni uthibitisho wa jitihada kubwa zinazofanywa na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga katika kuhakikisha mazingira safi, salama na yenye afya kwa wakazi wake, sambamba na kutekeleza kwa vitendo mikakati ya kitaifa ya usafi wa mazingira.
Manispaa inaendelea kuwashukuru wananchi wote kwa ushirikiano wao wa dhati na inawaomba kuendeleza juhudi za usafi wa mazingira kwa ustawi wa jamii na vizazi vijavyo.
Tanesco S, Mwanza Road
Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga
Simu: +255-28-2763213
Simu ya Mkononi: 0759 023 788
Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz
Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga