• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MANISPAA YA SHINYANGA YAJIPANGA KUPAMBANA NA UKATILI NA WATOTO WA MITAANI

Posted on: June 19th, 2025

Katika kuhakikisha ustawi, ulinzi na usalama wa watoto unaimarika katika Manispaa ya Shinyanga, shirika lisilo la kiserikali la Railway Children Africa limeendesha mafunzo maalum kwa wadau wa sekta ya ustawi wa jamii na ulinzi wa mtoto. Mafunzo haya yanalenga kuongeza uelewa wa namna ya kushughulikia tatizo la ukatili wa kijinsia pamoja na ongezeko la watoto wa mitaani.


Mafunzo hayo yamefanyika leo, Juni 19, 2025, katika Ukumbi wa Mikutano wa Lewis Kalinjuna, yakihusisha maafisa ustawi wa jamii, vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja na wadau wa maendeleo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi uanzishwaji wa dawati la huduma za ustawi wa jamii katika vituo vya mabasi, mradi unaolenga kutoa huduma za kijamii katika vituo vya mabasi, ambapo watoto wanaoishi mitaani hukutanishwa kwa wingi.


Akizungumza katika mafunzo haya Meneja wa Mradi kutoka Railway Children Africa Bi. Irene Wampembe, amesema shirika hilo limejikita zaidi kutoa elimu na msaada kwa watoto wanaoishi mitaani, hususani katika maeneo ya vituo vya mabasi ambako hukusanyika watoto kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi, huku akiongeza kuwa maeneo hayo yameonekana kuwa kiini cha kuongezeka kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.


Awali mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg. Revocatus Lutunda akifungua rasmi mafunzo hayo, amesema swala la ulizi na usalama wa mtoto ni la jamii nzima hivyo jamii inatakiwa kushirikiana ili kukomesha ongezeko la Watoto wa mtaani.


Naye, Afisa Ustawi dawati la ustawi wa jamii standi ya mabasi Manyoni, Bi. Penuela Samwel, ameeleza kuwa mpaka sasa, watoto 18 na watu wazima 20 wamepatiwa huduma mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuwaunganisha tena na familia zao. Huku akiwahimiza wazazi na walezi kuendelea kuwalea watoto katika maadili mema.


Katika kuunga mkono juhudi za utekelezaji wa mradi huo, Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa tayari imefungua ofisi ndogo katika kituo kikuu cha mabasi cha Mkoa wa Shinyanga, kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma za kijamii na kusaidia shirika kutekeleza majukumu yake ipasavyo.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • BOTI MPYA YA UOKOAJI ZIWA VICTORIA YAWASILI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 25, 2025
  • MANISPAA YA SHINYANGA YASAINI MIKATABA YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA MIJI TANZANIA.

    June 25, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI

    June 24, 2025
  • SALAMU ZA SHUKRANI

    June 24, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga