• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MAADHIMISHO SIKU YA WAFANYAKAZI 'MEI MOSI' MKOA WA SHINYANGA

Posted on: May 1st, 2022

SHIRIKISHO la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) mkoani Shinyanga, limeadhimisha siku ya wafanyakazi Mei mosi, huku likibainisha changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili watumishi wa umma na Sekta binafsi.

Maadhimisho yao yamefanyika leo Mei 1, 2022 katika viwanja vya michezo CCM Kambarage Manispaa ya Shinyanga, huku mgeni Rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema.

Akihutubia kwenye Maadhimisho hayo, Mjema amewataka watumishi wa Serikali mkoani humo, kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kujituma, na kusimamia miradi ya maendeleo kikamilifu ili itekelezwe kwa ubora.

"Malipo kwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan ni kufanya kazi kwa bidii na kutumikia wananchi ipasavyo pamoja na kusimamia vyema miradi ya kimkakati", alisema Mjema.

Aidha, aliwataka pia watumishi wa umma kulisimamia vyema zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kwa weledi mkubwa, ambalo litafanyika Agosti 23 mwaka huu ili malengo yaliyokusudiwa yafanikiwe na kuwasihi wananchi wakati wa zoezi hilo wajitokeze kwa wingi kuhesabiwa.

Katika hatua nyingine, alisema changamoto zote ambazo zimewasilishwa kwenye maadhimisho hayo, zile ambazo zipo ndani ya uwezo wake atazitafutia ufumbuzi, na zilizo nje ya uwezo wake za Kitaifa ataziwasilisha kwenye mamlaka husika.

Mjema pia alimwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Zuwena Omary, kushughulikia malalamiko yote ya Sekta binafsi juu ya wafanyakazi wao ndazi ya mwezi mmoja, ambayo yametolewa na Shirikisho hilo la vyama vya wafanyakazi (TUCTA), na watakaokaidi kutii maagizo ya Serikali watachuliwe hatua.

“Sekta binafsi inavyofanya juu ya wafanyakazi wao ni kinyume cha Sheria za ajira hili tutalishughulikia,”alisema Mjema.

Awali Mratibu wa TUCTA Mkoa wa Shinyanga Lazaro Mnjeja, akisoma Risala, alibainisha changamoto ambazo zinawakabili wafanyakazi wa Sekta binafsi, kuwa waajiri hawawapatii mikataba ya ajira, kuwazuia kujiunga na vyama vya wafanyakazi, hawapeleki michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii na hawatoi hati za malipo ya mishahara.

Alitaja changamoto zingine ambazo zinawakabili pia na wafanyakazi wa Sekta za umma na binafsi, kuwa ni ucheleweshwaji wa mafao kwa wastaafu, kutolipwa madai ya Likizo, uhamisho, kutopandishwa madaraja na mapunjo ya mishahara.

Pia aliiomba Serikali, wamiliki wa makampuni binafsi na viwanda wazingatie uboreshaji wa mishahara na maslahi kwa wafanyakazi ili iendane na kupanda kwa gharama za maisha.

“Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei mosi mwaka huu inatokana na hali halisi ya maisha ya wafanyakazi, kutokana na uwepo wa mishahara midogo na maslahi duni yasiyokidhi hali na gharama za maisha kwa sasa, hivyo tunaomba mishahara iongezwe, ”alisema Mnjema.

Wafanyakazi wakiwa kwenye maandamano kutoka Shirika la Posta kuelekea kwenye viwanja vya CCM Kambarage kuadhimisha siku ya wafanyakazi Meimosi.

Maandamano yakiendelea.

Burudani za mbio za Baiskeli katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei mosi mkoani Shinyanga.

Wafanyakazi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya Meimosi mkoani Shinyanga.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura akiwa kwenye maadhimisho ya siku ya Meimosi.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema, (kushoto) akimkabidhi cheti cha Pongezi Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura kweye maadhimisho hayo ya siku ya wafanyakazi Meimosi.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema, (kushoto) akimkabidhi cheti cha Pongezi Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama Anderson Msumba kweye maadhimisho hayo ya siku ya wafanyakazi Meimosi


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga