- Mwanzo
- Kuhusu sisi
- Utawala
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma Zetu
- Madiwani
- Miradi
- Machapisho
- Kituo cha Habari
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imepongezwa kwa kupata hati safi katika ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ulioishia Juni 30, 2024. Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, wakati wa mkutano maalumu wa baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili taarifa za majibu ya hoja zilizoibuliwa na CAG, kikao kilichofanyika leo, Juni 12, 2025.
Akizungumza katika mkutano huo, DC Mtatiro amesema hati safi hiyo ni kielelezo cha usimamizi mzuri wa rasilimali za umma na ushirikiano imara kati ya uongozi wa Manispaa na Baraza la Madiwani.
“Hati hii ni uthibitisho kuwa Manispaa ya Shinyanga, kwa kushirikiana na Baraza la Madiwani, inafanya kazi kwa ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, matumizi sahihi ya fedha, na utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Hoja zote zilizobaki ni nyepesi na zinaweza kutatuliwa kwa haraka. Natoa siku saba tu hoja zote ziwe zimejibiwa kikamilifu,” amesema DC Mtatiro.
Awali, akiwasilisha taarifa ya ukaguzi Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani wa Manispaa ya shinyanga, CPA Peter Tarimo, amesema jumla ya hoja 31 ziliibuliwa na CAG, ambapo tayari hoja 3 zimetekelezwa kikamilifu, Halmashauri inaendelea kushughulikia hoja zilizobaki kwa kuwasilisha majibu pamoja na vielelezo kwa Mkaguzi Mkuu wa Nje kwa ajili ya uhakiki.
Kwa upande wake, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Nje wa Mkoa wa Shinyanga, Ndg. Yusuph Mabwe, ameipongeza Manispaa kwa ushirikiano mzuri na Ofisi ya CAG mkoa katika kushughulikia hoja mbalimbali,
Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Elias Masumbuko, ameeleza kuwa mwaka 2020 Manispaa ilikadiriwa kukusanya Shilingi Bilioni 3, lakini kutokana na mikakati madhubuti iliyowekwa na wataalamu wa halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani, makusanyo ya mwaka 2024 yameongezeka hadi zaidi ya Shilingi Bilioni 6. Huku akitumia fursa hiyo kumpongeza pia Mkurugenzi wa Manispaa kwa juhudi na mikakati yake ya kuhakikisha miradi viporo inakamilika.
Tanesco S, Mwanza Road
Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga
Simu: +255-28-2763213
Simu ya Mkononi: 0759 023 788
Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz
Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga