• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

DC MBONEKO AKABIDHI MKOPO WA MIL 156.4 KWA VIKUNDI MAALUM

Posted on: September 28th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko amekabidhi Mikopo ya Ths. Mil 156.4 (Tsh. 156, 454,000/=) iliyotolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa Vikundi 11 vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu kutoka kata mbalimbali ikiwa ni sehemu ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashari kwa kipindi cha mwezi Aprili hadi Juni 2021/2022.

Mbali na kukabidhi mkopo huo, Mboneko pia amekabidhi baadhi ya vifaa vya usafi kwa vikundi ambavyo vilipatiwa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani kutoka Halmashauri.

Akizungumza wakati wa kukabidhi Mikopo hiyo, Mboneko amewataka wanakikundi hao kwenda kutumia mikopo kwa malengo yaliyokusudiwa na kurejesha kwa wakati ili vikundi vingine vipatiwe mkopo huo.

“Fedha hizi tunazowapa zikafanye kazi kweli kweli ili muwa mfano, nendeni mkafanye kazi kwa ushirikiano na mshikamano. Na endapo mtapata changamoto toeni taarifa. Unapopata changamoto sema”,amesema Mboneko.

“Nanyi Maafisa Maendeleo ya jamii hakikisheni mnasimamia vikundi hivi na muwape elimu namna ya kuendeleza miradi yao”,amesema Mboneko.

Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Elias Ramadhani Masumbuko amesema halmashauri hiyo itaendelea kutoa mikopo kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwani lengo ni kuwezesha wananchi wapige hatua kiuchumi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, Dkt. Jomaary Satura, amesema Halmashauri imenunua eneo kwa ajili ya Wajasiriamali wa Kitangili ili kuwawezesha kufanya shughuli zao na kuhakikisha vikundi vyote vinanufaika na mikopo.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, John Tesha amesema kikundi cha NDEIMA wamekipatia mkopo wa Shilingi 80,454,000/= pamoja kukieleza kufanya shughuli zao ndani ya eneo hilo lililonunuliwa na Halmashauri kwa muda wa miaka mitatu.

Mbali na kikundi cha NDEIMA pia wametoa mikopo kwa vikundi vingine 10 vikiwemo vikundi vine vya watu wenye ulemavu hivyo kufanya idadi ya vikundi vilivyopewa mikopo kuwa 11 vyote vikipata mkopo wa jumla ya shilingi milioni 156.4.

“Nitumie nafasi hii kuwakumbusha wanavikundi wote wanaokopeshwa na wale waliokwishakopeshwa wakumbuke kuwa mikopo hii wanayopatiwa lazima ikatekeleze miradi iliyoombwa na siyo vinginevyo. Kutotekeleza miradi waliyoombea mikopo au kubadilisha miradi iliyoombewa mikopo ni kinyume cha sheria na watachukuliwa hatua kali. Na vikundi ambavyo havitarejesha mikopo navyo vitachukuliwa hatua za kisheria”,amesema.

Mikopo hiyo imekabidhiwa Jumanne ya Septemba 27, 2022 katika kata ya Kitangili, eneo la ghala la kuhifadhia mazao lililonunuliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ambalo ndani yake kuna mashine ya kukoboa nafaka, visima vya maji, banda la kufugia kuku, ofisi ndogo, wanyama na mabwawa ya kufugia samaki linalosimamiwa na Muunganiko wa vikundi vitatu vya Wanawake vya Ndembezi, Ibadakuli na Masekelo ambavyo kwa jina moja vinajulikana kama NDEIMA.



Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • MHE. MWEBEA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MANISPAA YA SHINYANGA.

    June 05, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO OPD KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUKAMILIKA

    June 03, 2025
  • MUONEKANO WA JENGO LA UTAWALA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA KIPINDI CHA UJENZI NA BAADA YA KUMALIZA UJENZI

    June 02, 2025
  • WANAFUNZI KUTOKA SHULE 20 ZA MANISPAA YA SHINYANGA WAKUTANA KUBADILISHANA UJUZI ILI KUBORESHA TAALUMA.

    May 17, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga